< Giobbe 34 >

1 Elihu riprese a parlare e disse:
Kisha Elihu akasema:
2 “O voi savi, ascoltate le mie parole! Voi che siete intelligenti, prestatemi orecchio!
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 Poiché l’orecchio giudica dei discorsi, come il palato assapora le vivande.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 Scegliamo quello ch’è giusto, riconosciamo fra noi quello ch’è buono.
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 Giobbe ha detto: “Sono giusto, ma Dio mi nega giustizia;
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 ho ragione, e passo da bugiardo; la mia ferita è incurabile, e sono senza peccato”.
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 Dov’è l’uomo che al par di Giobbe tracanni gli empi scherni come l’acqua,
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 cammini in compagnia de’ malfattori, e vada assieme con gli scellerati?
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 Poiché ha detto: “Non giova nulla all’uomo l’avere il suo diletto in Dio”.
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 Ascoltatemi dunque, o uomini di senno! Lungi da Dio il male, lungi dall’Onnipotente l’iniquità!
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 Poich’egli rende all’uomo secondo le sue opere, e fa trovare a ognuno il salario della sua condotta.
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 No, di certo Iddio non commette ingiustizie! l’Onnipotente non perverte il diritto.
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 Chi gli ha dato il governo della terra? Chi ha affidato l’universo alla sua cura?
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 S’ei non ponesse mente che a sé stesso, se ritirasse a sé il suo spirito e il suo soffio,
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 ogni carne perirebbe d’un tratto, l’uomo ritornerebbe in polvere.
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 Se tu se’ intelligente, ascolta questo, porgi orecchio alla voce delle mie parole.
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 Uno che odiasse la giustizia potrebbe governare? E osi tu condannare il Giusto, il Potente,
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 che chiama i re “uomini da nulla” e i principi: “scellerati”?
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 che non porta rispetto all’apparenza de’ grandi, che non considera il ricco più del povero, perché son tutti opera delle sue mani?
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 In un attimo, essi muoiono; nel cuor della notte, la gente del popolo è scossa e scompare, i potenti son portati via, senza man d’uomo.
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 Perché Iddio tien gli occhi aperti sulle vie de’ mortali, e vede tutti i lor passi.
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 Non vi son tenebre, non v’è ombra di morte, ove possa nascondersi chi opera iniquamente.
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 Dio non ha bisogno d’osservare a lungo un uomo per trarlo davanti a lui in giudizio.
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 Egli fiacca i potenti, senza inchiesta; e ne stabilisce altri al loro posto;
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 poich’egli conosce le loro azioni; li abbatte nella notte, e son fiaccati;
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 li colpisce come dei malvagi, in presenza di tutti,
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 perché si sono sviati da lui e non hanno posto mente ad alcuna delle sue vie;
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 han fatto salire a lui il gemito del povero, ed egli ha dato ascolto al gemito degli infelici.
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 Quando Iddio dà requie chi lo condannerà? Chi potrà contemplarlo quando nasconde il suo volto a una nazione ovvero a un individuo,
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 per impedire all’empio di regnare, per allontanar dal popolo le insidie?
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 Quell’empio ha egli detto a Dio: “Io porto la mia pena, non farò più il male,
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 mostrami tu quel che non so vedere; se ho agito perversamente, non lo farò più”?
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 Dovrà forse Iddio render la giustizia a modo tuo, che tu lo critichi? Ti dirà forse: “Scegli tu, non io, quello che sai, dillo”?
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 La gente assennata e ogni uomo savio che m’ascolta, mi diranno:
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 “Giobbe parla senza giudizio, le sue parole sono senza intendimento”.
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 Ebbene, sia Giobbe provato sino alla fine! poiché le sue risposte son quelle degli iniqui,
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 poiché aggiunge al peccato suo la ribellione, batte le mani in mezzo a noi, e moltiplica le sue parole contro Dio”.
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

< Giobbe 34 >