< 1 Cronache 24 >

1 Le classi dei figliuoli d’Aaronne furono queste. Figliuoli d’Aaronne: Nadab, Abihu, Eleazar e Ithamar.
Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Nadab e Abihu morirono prima del loro padre, e non ebbero figliuoli; Eleazar e Ithamar esercitarono il sacerdozio.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
3 Or Davide, con Tsadok de’ figliuoli di Eleazar, e con Ahimelec de’ figliuoli d’Ithamar, classificò i figliuoli d’Aaronne secondo il servizio che doveano fare.
Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
4 Tra i figliuoli di Eleazar si trovarono più capi di famiglie che tra i figliuoli d’Ithamar; e furon divisi così: per i figliuoli di Eleazar, sedici capi di famiglie patriarcali; per i figliuoli d’Ithamar, otto capi delle loro famiglie patriarcali.
Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
5 La classificazione fu fatta a sorte, tanto per gli uni quanto per gli altri; perché v’erano dei principi del santuario e de’ principi di Dio tanto tra i figliuoli d’Eleazar quanto tra i figliuoli d’Ithamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
6 Scemaia, figliuolo di Nathaneel, il segretario, ch’era della tribù di Levi, li iscrisse in presenza del re e dei principi, in presenza del sacerdote Tsadok, di Ahimelec, figliuolo di Ebiathar, e in presenza dei capi delle famiglie patriarcali dei sacerdoti e dei Leviti. Si tirò a sorte una casa patriarcale per Eleazar, e, proporzionalmente, per Ithamar.
Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
7 Il primo, designato dalla sorte, fu Jehoiarib; il secondo, Jedaia;
Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
8 il terzo, Harim; il quarto, Seorim;
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
9 il quinto, Malkija;
ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
10 il sesto, Mijamin; il settimo, Hakkots; l’ottavo, Abija;
ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
11 il nono, Jeshua; il decimo, Scecania;
ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
12 l’undecimo, Eliascib; il dodicesimo, Jakim;
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
13 il tredicesimo, Huppa; il quattordicesimo, Jescebeab;
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
14 il quindicesimo, Bilga; il sedicesimo, Immer;
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
15 il diciassettesimo, Hezir; il diciottesimo, Happitsets;
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
16 il diciannovesimo, Pethahia; il ventesimo, Ezechiele;
ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
17 il ventunesimo, Jakin; il ventiduesimo, Gamul;
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
18 il ventitreesimo, Delaia; il ventiquattresimo, Maazia.
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Così furono classificati per il loro servizio, affinché entrassero nella casa dell’Eterno secondo la regola stabilita per loro da Aaronne loro padre, e che l’Eterno, l’Iddio d’Israele, gli aveva prescritta.
Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 Quanto al rimanente de’ figliuoli di Levi, questi ne furono i capi. Dei figliuoli d’Amram: Shubael; de’ figliuoli di Shubael: Jehdia.
Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
21 Di Rehabia, de’ figliuoli di Rehabia: il capo Jscia.
Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
22 Degli Jtsehariti: Scelomoth; de’ figliuoli di Scelomoth: Jahath.
Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
23 Figliuoli di Hebron: Jerija, Amaria il secondo, Jahaziel il terzo, Jekameam il quarto.
Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
24 Figliuoli di Uzziel: Mica; de’ figliuoli di Mica: Shamir;
Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
25 fratello di Mica: Jscia; de’ figliuoli d’Jscia: Zaccaria.
Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
26 Figliuoli di Merari: Mahli e Musci, e i figliuoli di Jaazia, suo figliuolo,
Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
27 vale a dire i figliuoli di Merari, per il tramite di Jaazia suo figliuolo: Shoham, Zaccur e Ibri.
Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 Di Mahli: Eleazar, che non ebbe figliuoli.
Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
29 Di Kis: i figliuoli di Kis: Jerahmeel.
Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
30 Figliuoli di Musci: Mahli, Eder e Jerimoth. Questi sono i figliuoli dei Leviti secondo le loro case patriarcali.
Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
31 Anch’essi, come i figliuoli d’Aaronne, loro fratelli, tirarono a sorte in presenza del re Davide, di Tsadok, di Ahimelec e dei capi delle famiglie patriarcali dei sacerdoti e dei Leviti. Ogni capo di famiglia patriarcale tirò a sorte, nello stesso modo che il fratello, più giovane di lui.
Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.

< 1 Cronache 24 >