< Salmi 77 >

1 Salmo di Asaf, [dato] al Capo de' Musici, de' figliuoli di Iedutun LA mia voce [s'indirizza] a Dio, ed io grido; La mia voce [s'indirizza] a Dio, acciocchè egli mi porga l'orecchio.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 Nel giorno della mia distretta, io ho cercato il Signore; Le mie mani sono state sparse qua e là di notte, E non hanno avuta posa alcuna; L'anima mia ha rifiutato d'essere consolata.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 Io mi ricordo di Dio, e romoreggio; Io mi lamento, e il mio spirito è angosciato. (Sela)
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 Tu hai ritenuti gli occhi miei [in continue] vegghie; Io son tutto attonito, e non posso parlare.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 Io ripenso a' giorni antichi, Agli anni da lungo tempo passati.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 Io mi ricordo come [già] io sonava; Io medito nel mio cuore di notte, E lo spirito mio va investigando.
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 Il Signore [mi] rigetterà egli in perpetuo? E non [mi] gradirà egli [giammai] più?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 È la sua benignità venuta meno per sempre mai? È la [sua] parola mancata per ogni età?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Iddio ha egli dimenticato di aver pietà? Ha egli serrate per ira le sue compassioni? (Sela)
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 Io ho adunque detto: Se io son fiacco, Egli è perchè la destra dell'Altissimo è mutata.
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 Io mi rammemoro le opere del Signore; Perciocchè io mi riduco a memoria le tue maraviglie antiche;
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 E medito tutti i tuoi fatti, E ragiono delle tue operazioni.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 O Dio, le tue vie [si veggono] nel Santuario; Chi [è] dio grande, come Iddio?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 Tu [sei] l'Iddio che fai maraviglie; Tu hai fatta conoscere la tua forza fra i popoli.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 Tu hai, col tuo braccio, riscosso il tuo popolo; I figliuoli di Giacobbe e di Giuseppe. (Sela)
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 Le acque ti videro, o Dio; Le acque ti videro, [e] furono spaventate; Gli abissi eziandio tremarono.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 Le nubi versarono diluvi d'acque; I cieli tuonarono; I tuoi strali eziandio andarono attorno.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 Il suon de' tuoi tuoni [fu] per lo giro [del cielo]; I folgori alluminarono il mondo; La terra fu smossa, e tremò.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 La tua via [fu] per mezzo il mare, E il tuo sentiero per mezzo le grandi acque; E le tue pedate non furono riconosciute.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 Tu conducesti il tuo popolo, come una greggia, Per man di Mosè e d'Aaronne.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

< Salmi 77 >