< Salmi 48 >

1 Cantico di Salmo, de' figliuoli di Core IL Signore [è] grande, e molto glorioso Nella Città dell'Iddio nostro, [nel] monte della sua santità.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Il monte di Sion, il fondo verso il Settentrione, La Città del gran Re [È in] bella contrada, [è] la gioia di tutta la terra.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 Iddio [è] riconosciuto ne' palazzi di essa, per alta fortezza.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 Perciocchè ecco, i re si erano adunati, Ed erano tutti insieme passati oltre.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 Come prima [la] videro, furono attoniti, Si smarrirono, si affrettarono [a fuggire].
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Tremore li colse quivi; Doglia, come di donna che partorisce.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 [Furono rotti come] per lo vento orientale [Che] rompe le navi di Tarsis.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Come avevamo udito, così abbiam veduto, Nella Città del Signor degli eserciti, Nella Città dell'Iddio nostro; Iddio la stabilirà in perpetuo. (Sela)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 O Dio, noi abbiamo, chetamente aspettata la tua benignità Dentro al tuo Tempio.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 O Dio, quale [è] il tuo Nome, Tale [è] la tua lode, infino all'estremità della terra; La tua destra è piena di giustizia.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Il monte di Sion si rallegrerà, Le figliuole di Giuda festeggeranno, per li tuoi giudicii.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Circuite Sion, e andate attorno a lei, Contate le sue torri.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Ponete mente alle bastie, Mirate l'altezza de' suoi palazzi; Acciocchè [lo] raccontiate all'età a venire.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 Perciocchè questo Dio [è] il nostro Dio in sempiterno; Egli ci giuderà infino alla morte.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Salmi 48 >