< Salmi 4 >

1 Salmo di Davide, [dato] al Capo de' Musici, in su Neghinot QUANDO io grido, rispondimi, o Dio della mia giustizia; Quando io sono stato distretto, tu mi hai messo in largo; Abbi pietà di me, ed esaudisci la mia orazione.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
2 O uomini principali, infino a quando [sarà] la mia gloria in vituperio? [Infino a quando] amerete vanità, [E] andrete dietro a menzogna? (Sela)
Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 Or sappiate che il Signore si ha eletto un pietoso; Il Signore [mi] esaudirà quando io griderò a lui.
Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
4 Tremate, e non peccate; Ragionate nel cuor vostro, sopra i vostri letti, e restate. (Sela)
Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
5 Sacrificate sacrificii di giustizia, E confidatevi nel Signore.
Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
6 Molti dicono: Chi ci farà veder del bene? O Signore, alza la luce del tuo volto sopra noi.
Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 Tu mi hai data maggiore allegrezza nel cuore, che [non hanno quelli] Nel tempo [che] il lor frumento, e il lor mosto è moltiplicato.
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 Io mi coricherò in pace, ed [in pace] ancora dormirò; Perciocchè tu solo, Signore, mi fai abitare sicuramente.
Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.

< Salmi 4 >