< Salmi 2 >
1 PERCHÈ tumultuano le genti, E mormorano i popoli cose vane?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 I re della terra si ritrovano, Ed i principi consigliano insieme, Contro al Signore, e contro al suo Unto;
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 [Dicendo: ] Rompiamo i lor legami, E gettiam via da noi le lor funi.
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 Colui che siede ne' cieli[ne] riderà; Il Signore si befferà di loro.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Allora parlerà loro nella sua ira, E li renderà smarriti nel suo cruccio acceso;
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 [E dirà: ] Pur nondimeno ho io consacrato il mio Re Sopra Sion, monte della mia santità.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 Io spiegherò il decreto; Il Signore mi ha detto: Tu [sei] il mio figliuolo; Oggi io t'ho generato.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Chiedimi, ed io ti darò [per] eredità le genti, Ed i confini della terra [per] tua possessione.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Tu le fiaccherai con una verga di ferro; Tu le triterai come un testo di vasellaio.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Ora dunque, o re, siate savi; Giudici della terra, ricevete correzione.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Servite al Signore con timore, E gioite con tremore.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Baciate il figliuolo, che talora egli non si adiri, E che voi non periate [nella vostra] via, Quando l'ira sua si sarà pure un poco accesa. Beati tutti coloro che si confidano in lui.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.