< Salmi 148 >

1 ALLELUIA. Lodate il Signore dal cielo; Lodatelo ne' [luoghi] altissimi.
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Lodatelo [voi], suoi Angeli tutti. Lodatelo [voi], suoi eserciti.
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 Lodatelo, sole e luna; Lodatelo [voi], stelle lucenti tutte.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 Lodatelo [voi], cieli de' cieli; E [voi], acque che [siete] di sopra al cielo.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 [Tutte queste cose] lodino il nome del Signore; Perciocchè al suo comandamento furono create.
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 Ed egli le ha stabilite per sempre [ed] in perpetuo; Egli ne ha fatto uno statuto, il qual non trapasserà giammai.
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Lodate il Signore della terra. Balene, ed abissi tutti;
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 Fuoco, e gragnuola; neve, e vapore, [E] vento tempestoso ch'eseguisce la sua parola;
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 Monti, e colli tutti; Alberi fruttiferi, e cedri tutti;
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 Fiere, e bestie domestiche tutte; Rettili, ed uccelli alati;
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 Re della terra, e popoli tutti; Principi, e rettori della terra tutti;
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 Giovani, ed anche vergini; Vecchi, e fanciulli;
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 Lodino il Nome del Signore; Perciocchè il Nome di lui solo è innalzato; La sua maestà [è] sopra la terra, e [sopra] il cielo.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Ed ha alzato un corno al suo popolo, Il che [è materia di] lode a tutti i suoi santi: A' figliuoli d'Israele, suo popolo prossimo. Alleluia.
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.

< Salmi 148 >