< Salmi 135 >

1 ALLELUIA. Lodate il Nome del Signore; Lodate[lo, voi] servitori del Signore;
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 Che state nella Casa del Signore, Ne' cortili della Casa del nostro Dio.
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Lodate il Signore; perciocchè il Signore [è] buono; Salmeggiate al suo Nome, perciocchè [è] amabile.
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 Conciossiachè il Signore si abbia eletto Giacobbe [Ed] Israele per suo tesoro riposto.
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 Certo io conosco che il Signore [è] grande, E che il nostro Signore [è maggiore] di tutti gl'iddii.
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 Il Signore fa tutto ciò che gli piace In cielo ed in terra; Ne' mari, ed [in] tutti gli abissi.
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 Egli fa salire i vapori dall'estremità dalle terra; Egli fa i lampi per la pioggia; Egli trae fuori il vento da' suoi tesori.
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 [Egli è quel] che percosse i primogeniti di Egitto, Così degli uomini, come degli animali.
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 Che mandò segni e prodigi, in mezzo di te, o Egitto; Sopra Faraone, e sopra tutti i suoi servitori.
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Che percosse nazioni grandi, Ed uccise re potenti;
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 Sihon, re degli Amorrei, E Og, re di Basan, E i re di tutti i regni di Canaan;
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 E diede i lor paesi per eredità, Per eredità ad Israele, suo popolo.
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 O Signore, il tuo Nome [è] in eterno; O Signore, la memoria di te [è] per ogni età.
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 Quando il Signore avrà fatti i suoi giudicii sopra il suo popolo, Egli si pentirà per amor de' suoi servitori.
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 Gl'idoli delle genti[sono] argento ed oro, Opera di mani d'uomini;
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 Hanno bocca, e non parlano; Hanno occhi, e non veggono;
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 Hanno orecchi, e non odono; [Ed] anche non hanno fiato alcuno nella lor bocca.
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 Simili ad essi sieno quelli che li fanno; Chiunque in essi si confida.
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 Casa d'Israele, benedite il Signore; Casa d'Aaronne, benedite il Signore.
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 Casa di Levi, benedite il Signore; [Voi] che temete il Signore, beneditelo.
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 Benedetto [sia] da Sion il Signore, Che abita in Gerusalemme. Alleluia.
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Salmi 135 >