< Giobbe 29 >
1 E GIOBBE riprese il suo ragionamento, e disse:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Oh! fossi io pure come a' mesi di prima, Come al tempo che Iddio mi guardava!
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Quando egli faceva rilucere la sua lampana sopra il mio capo, E [quando] io camminava al suo lume, per mezzo le tenebre;
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Come io era al tempo della mia giovanezza, Mentre il consiglio di Dio governava il mio tabernacolo;
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Mentre l'Onnipotente [era] ancora meco, [E] i miei famigli mi [erano] d'intorno;
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Mentre io lavava i miei passi nel burro, E le rocce versavano presso di me de' ruscelli d'olio.
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Quando io andava fuori alla porta per la città, [O] mi faceva porre il mio seggio in su la piazza,
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 I fanciulli, veggendomi, si nascondevano; E i vecchi si levavano, e stavano in piè;
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 I principali si rattenevano di parlare, E si mettevano la mano in su la bocca;
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 La voce de' rettori era celata, E la lor lingua era attaccata al lor palato;
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 L'orecchio che [mi] udiva mi celebrava beato; L'occhio che [mi] vedeva mi rendeva testimonianza;
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Perciocchè io liberava il povero che gridava, E l'orfano che non avea chi l'aiutasse.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 La benedizione di chi periva veniva sopra me; Ed io faceva cantare il cuor della vedova.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Io mi vestiva di giustizia, ed [ella altresì] mi rivestiva; La mia dirittura [mi era] come un ammanto, e come una benda.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Io era occhi al cieco, E piedi allo zoppo.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 Io [era] padre a' bisognosi, E investigava la causa che mi era sconosciuta.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 E rompeva i mascellari al perverso, E gli faceva gittar la preda d'infra i denti.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Onde io diceva: Io morrò nel mio nido, E moltiplicherò i [miei] giorni come la rena.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 La mia radice [era] aperta alle acque, E la rugiada era tutta la notte in su i miei rami.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 La mia gloria si rinnovava in me, E il mio arco si rinforzava in mano mia.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 [Altri] mi ascoltava, ed aspettava [che io avessi parlato]; E taceva al mio consiglio.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Dopo che io avea parlato, niuno replicava; E i miei ragionamenti stillavano sopra loro.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Essi mi aspettavano come la pioggia, Ed aprivano la bocca, [come] dietro alla pioggia della stagione della ricolta.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 [Se] io rideva verso loro, essi nol credevano, E non facevano scader la chiarezza della mia faccia.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 [Se] mi piaceva d'andar con loro, io sedeva in capo, Ed abitava con loro come un re fra le [sue] schiere, E come una persona che consola quelli che fanno cordoglio.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.