< Genesi 23 >

1 OR la vita di Sara fu di cenventisett'anni. [Questi furono] gli anni della vita di Sara.
Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba. Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara.
2 E Sara morì in Chiriat-Arba, [ch'è] Hebron, nel paese di Canaan, ed Abrahamo entrò, per far duolo di Sara, e per piangerla.
Sara akafa katika Kiriathi Arba, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abraham akaomboleza na kumlilia Sara.
3 Poi Abrahamo si levò d'appresso al suo morto, e parlò a' figliuoli di Het, dicendo:
Kisha Abraham akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa, akanena na watoto wa kiume wa Hethi, akisema,
4 Io [sono] straniere ed avveniticcio appresso di voi; datemi la possessione di una sepoltura appo voi; acciocchè io seppellisca il mio morto, e mel [levi] d'innanzi.
“Mimi ni mgeni kati yenu. Tafadhari nipatieni mahali pa kuzikia miongoni mwenu, ili kwamba niweze kuzika wafu wangu.”
5 E i figliuoli di Het risposero ad Abrahamo, dicendogli:
Wana wa Hethi wakamjibu Abraham, wakasema,
6 Signor mio, ascoltaci: Tu [sei] per mezzo noi un principe divino; seppellisci il tuo morto nella più scelta delle nostre sepolture; niuno di noi ti rifiuterà la sua sepoltura, che tu non [vi] seppellisca il tuo morto.
“Tusikilize, bwana wangu. Wewe ni mwana wa Mungu miongoni mwetu. Zika wafu wako katika makaburi yetu utakayochagua. Hakuna miongoni mwetu atakaye kuzuilia kaburi lake, kwa ajili ya kuzikia wafu wako.”
7 Ed Abrahamo si levò, e s'inchinò al popolo del paese, a' figliuoli di Het; e parlò con loro, dicendo:
Abraham akainuka na kusujudu chini kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi.
8 Se voi avete nell'animo che io seppellisca il mio morto, [e mel levi] d'innanzi, ascoltatemi: Intercedete per me appo Efron, figliuolo di Sohar;
Akawaambia, akisema, “ikiwa mmekubali mimi kuzika wafu wangu, ndipo nisikilizeni, msihini Efroni mwana wa Sohari kwa ajili yangu.
9 che mi dia la spelonca di Macpela, che [è] sua, la quale [è] nell'estremità del suo campo; che me la dia per lo suo prezzo intiero, per possession di sepoltura fra voi.
Mwambieni aniuzie pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake. Kwa bei kamili aniuzie waziwazi mbele ya watu kama miliki ya kuzikia.”
10 Or Efron sedeva per mezzo i figliuoli di Het. Ed Efron Hitteo rispose ad Abrahamo, in presenza de' figliuoli di Het, di tutti coloro ch'entravano nella porta della sua città, dicendo:
Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi, hivyo Efroni Mhiti akamjibu Abraham alipowasikia wana wa Hethi, wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake, akasema,
11 No, signor mio; ascoltami: Io ti dono il campo; ti dono ancora la spelonca ch'[è] in esso; io te ne fo un dono, in presenza de' figliuoli del mio popolo; seppellisci[vi] il tuo morto.
“Hapana, bwana wangu, nisikilize. Ninakupatia shamba na pango ambalo limo ndani yake. Ninakupatia mbele ya wana wa watu wangu. Ninakupatia uzike wafu wako.”
12 Ed Abrahamo s'inchinò al popolo del paese;
Kisha Abraham akasujudu chini mbele ya watu wa nchi ile.
13 e parlò ad Efron, in presenza del popolo del paese, dicendo: Anzi se [così] ti [piace], ascoltami, ti prego: Io darò i danari del campo; prendili da me, ed io vi seppellirò il mio morto.
Akamwambia Efroni watu wa nchi ile wakisikiliza, akasema, ikiwa uko radhi, tafadhari nisikilize. Nitalipia shamba. Chukua fedha kwangu, na nitazika wafu wangu pale.”
14 Ed Efron rispose ad Abrahamo, dicendogli:
Efroni akamjibu Abraham, akisema,
15 Signor mio, ascoltami: Fra me e te che cosa [è] una terra di quattrocento sicli d'argento? seppellisci[vi] pure il tuo morto.
“Tafadhari bwana wangu, nisikilize. Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe? wazike wafu wako.”
16 Ed Abrahamo acconsentì ad Efron, e gli pagò i danari ch'egli gli avea detto, in presenza de' figliuoli di Het; [cioè] quattrocento sicli d'argento, correnti fra' mercatanti.
Abraham akamsikiliza Efroni na akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema mbele ya wana wa Helthi wakisikiliza, shekeli mia nne za fedha, kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara.
17 Così l'acquisto del campo di Efron, il quale [è] in Macpela, ch'[è] dirimpetto a Mamre, insieme con la spelonca che [è] in esso, e con tutti gli alberi ch'[erano] in esso campo, in tutti i suoi confini attorno attorno,
Kwa hiyo shamba la Efroni, lililokuwa katika Makpela, mbele ya Mamre, shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote iliyokuwamo ndani ya shamba na iliyokuwa mpakani ikatolewa
18 fu fermato ad Abrahamo, in presenza de' figliuoli di Het, fra tutti coloro ch'entravano nella porta della città di esso.
kwa Abraham kwa njia ya manunuzi mbele ya wana wa Hethi, na mbele ya wote waliokuja malangoni pa mji wake.
19 E dopo ciò, Abrahamo seppellì Sara, sua moglie, nella spelonca del campo di Macpela, ch'[è] dirimpetto a Mamre, ch'[è] Hebron, nel paese di Canaan.
Baada ya haya, Abraham akamzika Sara mkewe katika pango la shamba la Makpela, lililo mbele ya Mamre, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani.
20 Così l'acquisto di quel campo, e della spelonca ch'[è] in esso, fu fermato ad Abrahamo, per possession di sepoltura, dai figliuoli di Het.
Kwa hiyo shamba pamoja na pango likatolewa na wana wa Hethi kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia.

< Genesi 23 >