< Salmi 73 >
1 Quanto è buono Dio con i giusti, con gli uomini dal cuore puro! Salmo. Di Asaf.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 Per poco non inciampavano i miei piedi, per un nulla vacillavano i miei passi,
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 perché ho invidiato i prepotenti, vedendo la prosperità dei malvagi.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 Non c'è sofferenza per essi, sano e pasciuto è il loro corpo.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 Non conoscono l'affanno dei mortali e non sono colpiti come gli altri uomini.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Dell'orgoglio si fanno una collana e la violenza è il loro vestito.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Esce l'iniquità dal loro grasso, dal loro cuore traboccano pensieri malvagi.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 Scherniscono e parlano con malizia, minacciano dall'alto con prepotenza.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 Levano la loro bocca fino al cielo e la loro lingua percorre la terra.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Perciò seggono in alto, non li raggiunge la piena delle acque.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 Dicono: «Come può saperlo Dio? C'è forse conoscenza nell'Altissimo?».
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Ecco, questi sono gli empi: sempre tranquilli, ammassano ricchezze.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Invano dunque ho conservato puro il mio cuore e ho lavato nell'innocenza le mie mani,
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 poiché sono colpito tutto il giorno, e la mia pena si rinnova ogni mattina.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 Se avessi detto: «Parlerò come loro», avrei tradito la generazione dei tuoi figli.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Riflettevo per comprendere: ma fu arduo agli occhi miei,
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 finché non entrai nel santuario di Dio e compresi qual è la loro fine.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Ecco, li poni in luoghi scivolosi, li fai precipitare in rovina.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 Come sono distrutti in un istante, sono finiti, periscono di spavento!
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 Come un sogno al risveglio, Signore, quando sorgi, fai svanire la loro immagine.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Quando si agitava il mio cuore e nell'intimo mi tormentavo,
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 io ero stolto e non capivo, davanti a te stavo come una bestia.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Ma io sono con te sempre: tu mi hai preso per la mano destra.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Mi guiderai con il tuo consiglio e poi mi accoglierai nella tua gloria.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 Chi altri avrò per me in cielo? Fuori di te nulla bramo sulla terra.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 Vengono meno la mia carne e il mio cuore; ma la roccia del mio cuore è Dio, è Dio la mia sorte per sempre.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Ecco, perirà chi da te si allontana, tu distruggi chiunque ti è infedele.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Il mio bene è stare vicino a Dio: nel Signore Dio ho posto il mio rifugio, per narrare tutte le tue opere presso le porte della città di Sion.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.