< Salmi 69 >

1 Al maestro del coro. Su «I gigli». Di Davide. Salvami, o Dio: l'acqua mi giunge alla gola.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 Affondo nel fango e non ho sostegno; sono caduto in acque profonde e l'onda mi travolge.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 Sono sfinito dal gridare, riarse sono le mie fauci; i miei occhi si consumano nell'attesa del mio Dio.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 Più numerosi dei capelli del mio capo sono coloro che mi odiano senza ragione. Sono potenti i nemici che mi calunniano: quanto non ho rubato, lo dovrei restituire?
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 Dio, tu conosci la mia stoltezza e le mie colpe non ti sono nascoste.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Chi spera in te, a causa mia non sia confuso, Signore, Dio degli eserciti; per me non si vergogni chi ti cerca, Dio d'Israele.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Per te io sopporto l'insulto e la vergogna mi copre la faccia;
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 sono un estraneo per i miei fratelli, un forestiero per i figli di mia madre.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Poiché mi divora lo zelo per la tua casa, ricadono su di me gli oltraggi di chi ti insulta.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 Mi sono estenuato nel digiuno ed è stata per me un'infamia.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 Ho indossato come vestito un sacco e sono diventato il loro scherno.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Sparlavano di me quanti sedevano alla porta, gli ubriachi mi dileggiavano.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Ma io innalzo a te la mia preghiera, Signore, nel tempo della benevolenza; per la grandezza della tua bontà, rispondimi, per la fedeltà della tua salvezza, o Dio.
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Salvami dal fango, che io non affondi, liberami dai miei nemici e dalle acque profonde.
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 Non mi sommergano i flutti delle acque e il vortice non mi travolga, l'abisso non chiuda su di me la sua bocca.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Rispondimi, Signore, benefica è la tua grazia; volgiti a me nella tua grande tenerezza.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Non nascondere il volto al tuo servo, sono in pericolo: presto, rispondimi.
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Avvicinati a me, riscattami, salvami dai miei nemici.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 Tu conosci la mia infamia, la mia vergogna e il mio disonore; davanti a te sono tutti i miei nemici.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 L'insulto ha spezzato il mio cuore e vengo meno. Ho atteso compassione, ma invano, consolatori, ma non ne ho trovati.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Hanno messo nel mio cibo veleno e quando avevo sete mi hanno dato aceto.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 La loro tavola sia per essi un laccio, una insidia i loro banchetti.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 Si offuschino i loro occhi, non vedano; sfibra per sempre i loro fianchi.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Riversa su di loro il tuo sdegno, li raggiunga la tua ira ardente.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 La loro casa sia desolata, senza abitanti la loro tenda;
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 perché inseguono colui che hai percosso, aggiungono dolore a chi tu hai ferito.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Imputa loro colpa su colpa e non ottengano la tua giustizia.
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Siano cancellati dal libro dei viventi e tra i giusti non siano iscritti.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Io sono infelice e sofferente; la tua salvezza, Dio, mi ponga al sicuro.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Loderò il nome di Dio con il canto, lo esalterò con azioni di grazie,
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 che il Signore gradirà più dei tori, più dei giovenchi con corna e unghie.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Vedano gli umili e si rallegrino; si ravvivi il cuore di chi cerca Dio,
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 poiché il Signore ascolta i poveri e non disprezza i suoi che sono prigionieri.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 A lui acclamino i cieli e la terra, i mari e quanto in essi si muove.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 Perché Dio salverà Sion, ricostruirà le città di Giuda: vi abiteranno e ne avranno il possesso.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 La stirpe dei suoi servi ne sarà erede, e chi ama il suo nome vi porrà dimora.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.

< Salmi 69 >