< Salmi 44 >

1 Al maestro del coro. Dei figli di Core. Maskil. Dio, con i nostri orecchi abbiamo udito, i nostri padri ci hanno raccontato l'opera che hai compiuto ai loro giorni, nei tempi antichi.
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametueleza yale uliyotenda katika siku zao, siku za kale.
2 Tu per piantarli, con la tua mano hai sradicato le genti, per far loro posto, hai distrutto i popoli.
Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa na ukawapanda baba zetu, uliangamiza mataifa na kuwastawisha baba zetu.
3 Poiché non con la spada conquistarono la terra, né fu il loro braccio a salvarli; ma il tuo braccio e la tua destra e la luce del tuo volto, perché tu li amavi.
Sio kwa upanga wao waliipata nchi, wala si mkono wao uliwapatia ushindi; ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwapenda.
4 Sei tu il mio re, Dio mio, che decidi vittorie per Giacobbe.
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
5 Per te abbiamo respinto i nostri avversari nel tuo nome abbiamo annientato i nostri aggressori.
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
6 Infatti nel mio arco non ho confidato e non la mia spada mi ha salvato,
Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi;
7 ma tu ci hai salvati dai nostri avversari, hai confuso i nostri nemici.
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.
8 In Dio ci gloriamo ogni giorno, celebrando senza fine il tuo nome.
Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele.
9 Ma ora ci hai respinti e coperti di vergogna, e più non esci con le nostre schiere.
Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.
10 Ci hai fatti fuggire di fronte agli avversari e i nostri nemici ci hanno spogliati.
Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara.
11 Ci hai consegnati come pecore da macello, ci hai dispersi in mezzo alle nazioni.
Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa.
12 Hai venduto il tuo popolo per niente, sul loro prezzo non hai guadagnato.
Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.
13 Ci hai resi ludibrio dei nostri vicini, scherno e obbrobrio a chi ci sta intorno.
Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.
14 Ci hai resi la favola dei popoli, su di noi le nazioni scuotono il capo.
Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao.
15 L'infamia mi sta sempre davanti e la vergogna copre il mio volto
Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele,
16 per la voce di chi insulta e bestemmia, davanti al nemico che brama vendetta.
kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.
17 Tutto questo ci è accaduto e non ti avevamo dimenticato, non avevamo tradito la tua alleanza.
Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.
18 Non si era volto indietro il nostro cuore, i nostri passi non avevano lasciato il tuo sentiero;
Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
19 ma tu ci hai abbattuti in un luogo di sciacalli e ci hai avvolti di ombre tenebrose.
Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.
20 Se avessimo dimenticato il nome del nostro Dio e teso le mani verso un dio straniero,
Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
21 forse che Dio non lo avrebbe scoperto, lui che conosce i segreti del cuore?
je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?
22 Per te ogni giorno siamo messi a morte, stimati come pecore da macello.
Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
23 Svègliati, perché dormi, Signore? Dèstati, non ci respingere per sempre.
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
24 Perché nascondi il tuo volto, dimentichi la nostra miseria e oppressione?
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
25 Poiché siamo prostrati nella polvere, il nostro corpo è steso a terra. Sorgi, vieni in nostro aiuto;
Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.
26 salvaci per la tua misericordia.
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.

< Salmi 44 >