< Salmi 30 >

1 Salmo. Canto per la festa della dedicazione del tempio. Di Davide. Ti esalterò, Signore, perché mi hai liberato e su di me non hai lasciato esultare i nemici.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Signore Dio mio, a te ho gridato e mi hai guarito.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Signore, mi hai fatto risalire dagli inferi, mi hai dato vita perché non scendessi nella tomba. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Cantate inni al Signore, o suoi fedeli, rendete grazie al suo santo nome,
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 perché la sua collera dura un istante, la sua bontà per tutta la vita. Alla sera sopraggiunge il pianto e al mattino, ecco la gioia.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Nella mia prosperità ho detto: «Nulla mi farà vacillare!».
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Nella tua bontà, o Signore, mi hai posto su un monte sicuro; ma quando hai nascosto il tuo volto, io sono stato turbato.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 A te grido, Signore, chiedo aiuto al mio Dio.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 Quale vantaggio dalla mia morte, dalla mia discesa nella tomba? Ti potrà forse lodare la polvere e proclamare la tua fedeltà?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Ascolta, Signore, abbi misericordia, Signore, vieni in mio aiuto.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Hai mutato il mio lamento in danza, la mia veste di sacco in abito di gioia,
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 perché io possa cantare senza posa. Signore, mio Dio, ti loderò per sempre.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Salmi 30 >