< Salmi 23 >

1 Il Signore è il mio pastore: non manco di nulla; Salmo. Di Davide.
Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
2 su pascoli erbosi mi fa riposare ad acque tranquille mi conduce.
Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
3 Mi rinfranca, mi guida per il giusto cammino, per amore del suo nome.
hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Se dovessi camminare in una valle oscura, non temerei alcun male, perché tu sei con me. Il tuo bastone e il tuo vincastro mi danno sicurezza.
Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.
5 Davanti a me tu prepari una mensa sotto gli occhi dei miei nemici; cospargi di olio il mio capo. Il mio calice trabocca.
Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
6 Felicità e grazia mi saranno compagne tutti i giorni della mia vita, e abiterò nella casa del Signore per lunghissimi anni.
Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

< Salmi 23 >