< Salmi 148 >

1 Lodate il Signore dai cieli, lodatelo nell'alto dei cieli. Alleluia.
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Lodatelo, voi tutti, suoi angeli, lodatelo, voi tutte, sue schiere.
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 Lodatelo, sole e luna, lodatelo, voi tutte, fulgide stelle.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 Lodatelo, cieli dei cieli, voi acque al di sopra dei cieli.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 Lodino tutti il nome del Signore, perché egli disse e furono creati.
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 Li ha stabiliti per sempre, ha posto una legge che non passa.
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Lodate il Signore dalla terra, mostri marini e voi tutti abissi,
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 fuoco e grandine, neve e nebbia, vento di bufera che obbedisce alla sua parola,
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 monti e voi tutte, colline, alberi da frutto e tutti voi, cedri,
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 voi fiere e tutte le bestie, rettili e uccelli alati.
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 I re della terra e i popoli tutti, i governanti e i giudici della terra,
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 i giovani e le fanciulle, i vecchi insieme ai bambini
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 lodino il nome del Signore: perché solo il suo nome è sublime, la sua gloria risplende sulla terra e nei cieli.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Egli ha sollevato la potenza del suo popolo. E' canto di lode per tutti i suoi fedeli, per i figli di Israele, popolo che egli ama. Alleluia.
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.

< Salmi 148 >