< Proverbi 27 >
1 Non ti vantare del domani, perché non sai neppure che cosa genera l'oggi.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Ti lodi un altro e non la tua bocca, un estraneo e non le tue labbra.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 La pietra è greve, la sabbia è pesante, ma più dell'una e dell'altra lo è il fastidio dello stolto.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 La collera è crudele, l'ira è impetuosa; ma chi può resistere alla gelosia?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Meglio un rimprovero aperto che un amore celato.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Leali sono le ferite di un amico, fallaci i baci di un nemico.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 Gola sazia disprezza il miele; per chi ha fame anche l'amaro è dolce.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Come un uccello che vola lontano dal nido così è l'uomo che va errando lontano dalla dimora.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 Il profumo e l'incenso allietano il cuore, la dolcezza di un amico rassicura l'anima.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Non abbandonare il tuo amico né quello di tuo padre, non entrare nella casa di tuo fratello nel giorno della tua disgrazia. Meglio un amico vicino che un fratello lontano.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Sii saggio, figlio mio, e allieterai il mio cuore e avrò di che rispondere a colui che mi insulta.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 L'accorto vede il pericolo e si nasconde, gli inesperti vanno avanti e la pagano.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Prendigli il vestito perché si è fatto garante per uno straniero e tienilo in pegno per gli sconosciuti.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 Benedire il prossimo di buon mattino ad alta voce gli sarà imputato come una maledizione.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 Il gocciolar continuo in tempo di pioggia e una moglie litigiosa, si rassomigliano:
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 chi la vuol trattenere, trattiene il vento e raccoglie l'olio con la mano destra.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Il ferro si aguzza con il ferro e l'uomo aguzza l'ingegno del suo compagno.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 Il guardiano di un fico ne mangia i frutti, chi ha cura del suo padrone ne riceverà onori.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Come un volto differisce da un altro, così i cuori degli uomini differiscono fra di loro.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Come gli inferi e l'abisso non si saziano mai, così non si saziano mai gli occhi dell'uomo. (Sheol )
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
21 Come il crogiuolo è per l'argento e il fornello per l'oro, così l'uomo rispetto alla bocca di chi lo loda.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Anche se tu pestassi lo stolto nel mortaio tra i grani con il pestello, non scuoteresti da lui la sua stoltezza.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Preòccupati del tuo gregge, abbi cura delle tue mandrie,
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 perché non sono perenni le ricchezze, né un tesoro si trasmette di generazione in generazione.
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 Si toglie il fieno, apparisce l'erba nuova e si raccolgono i foraggi dei monti;
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 gli agnelli ti danno le vesti e i capretti il prezzo per comprare un campo,
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 le capre latte abbondante per il cibo e per vitto della tua famiglia. e per mantenere le tue schiave.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.