< Proverbi 23 >
1 Quando siedi a mangiare con un potente, considera bene che cosa hai davanti;
Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2 mettiti un coltello alla gola, se hai molto appetito.
na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3 Non desiderare le sue ghiottonerie, sono un cibo fallace.
Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4 Non affannarti per arricchire, rinunzia a un simile pensiero;
Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5 appena vi fai volare gli occhi sopra, essa gia non è più: perché mette ali come aquila e vola verso il cielo.
Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6 Non mangiare il pane di chi ha l'occhio cattivo e non desiderare le sue ghiottonerie,
Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7 perché come chi calcola fra di sé, così è costui; ti dirà: «Mangia e bevi», ma il suo cuore non è con te.
maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8 Il boccone che hai mangiato rigetterai e avrai sprecato le tue parole gentili.
Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9 Non parlare agli orecchi di uno stolto, perché egli disprezzerà le tue sagge parole.
Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
10 Non spostare il confine antico, e non invadere il campo degli orfani,
Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
11 perché il loro vendicatore è forte, egli difenderà la loro causa contro di te.
maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
12 Piega il cuore alla correzione e l'orecchio ai discorsi sapienti.
Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 Non risparmiare al giovane la correzione, anche se tu lo batti con la verga, non morirà;
Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14 anzi, se lo batti con la verga, lo salverai dagli inferi. (Sheol )
Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol )
15 Figlio mio, se il tuo cuore sarà saggio, anche il mio cuore gioirà.
Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16 Esulteranno le mie viscere, quando le tue labbra diranno parole rette.
sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17 Il tuo cuore non invidi i peccatori, ma resti sempre nel timore del Signore,
Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18 perché così avrai un avvenire e la tua speranza non sarà delusa.
Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 Ascolta, figlio mio, e sii saggio e indirizza il cuore per la via retta.
Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 Non essere fra quelli che s'inebriano di vino, né fra coloro che son ghiotti di carne,
Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 perché l'ubriacone e il ghiottone impoveriranno e il dormiglione si vestirà di stracci.
maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 Ascolta tuo padre che ti ha generato, non disprezzare tua madre quando è vecchia.
Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 Acquista il vero bene e non cederlo, la sapienza, l'istruzione e l'intelligenza.
Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 Il padre del giusto gioirà pienamente e chi ha generato un saggio se ne compiacerà.
Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25 Gioisca tuo padre e tua madre e si rallegri colei che ti ha generato.
Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26 Fà bene attenzione a me, figlio mio, e tieni fisso lo sguardo ai miei consigli:
Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27 una fossa profonda è la prostituta, e un pozzo stretto la straniera.
Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28 Essa si apposta come un ladro e aumenta fra gli uomini il numero dei perfidi.
Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29 Per chi i guai? Per chi i lamenti? Per chi i litigi? Per chi i gemiti? A chi le percosse per futili motivi? A chi gli occhi rossi?
Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30 Per quelli che si perdono dietro al vino e vanno a gustare vino puro.
Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31 Non guardare il vino quando rosseggia, quando scintilla nella coppa e scende giù piano piano;
Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32 finirà con il morderti come un serpente e pungerti come una vipera.
Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33 Allora i tuoi occhi vedranno cose strane e la tua mente dirà cose sconnesse.
Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34 Ti parrà di giacere in alto mare o di dormire in cima all'albero maestro.
Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
35 «Mi hanno picchiato, ma non sento male. Mi hanno bastonato, ma non me ne sono accorto. Quando mi sveglierò? Ne chiederò dell'altro».
Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”