< Giobbe 6 >
2 Se ben si pesasse il mio cruccio e sulla stessa bilancia si ponesse la mia sventura...
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 certo sarebbe più pesante della sabbia del mare! Per questo temerarie sono state le mie parole,
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 perché le saette dell'Onnipotente mi stanno infitte, sì che il mio spirito ne beve il veleno e terrori immani mi si schierano contro!
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Raglia forse il somaro con l'erba davanti o muggisce il bue sopra il suo foraggio?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Si mangia forse un cibo insipido, senza sale? O che gusto c'è nell'acqua di malva?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Ciò che io ricusavo di toccare questo è il ributtante mio cibo!
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Oh, mi accadesse quello che invoco, e Dio mi concedesse quello che spero!
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 Volesse Dio schiacciarmi, stendere la mano e sopprimermi!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Ciò sarebbe per me un qualche conforto e gioirei, pur nell'angoscia senza pietà, per non aver rinnegato i decreti del Santo.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 Qual la mia forza, perché io possa durare, o qual la mia fine, perché prolunghi la vita?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 La mia forza è forza di macigni? La mia carne è forse di bronzo?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Non v'è proprio aiuto per me? Ogni soccorso mi è precluso?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 A chi è sfinito è dovuta pietà dagli amici, anche se ha abbandonato il timore di Dio.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 I miei fratelli mi hanno deluso come un torrente, sono dileguati come i torrenti delle valli,
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 i quali sono torbidi per lo sgelo, si gonfiano allo sciogliersi della neve,
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 ma al tempo della siccità svaniscono e all'arsura scompaiono dai loro letti.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Deviano dalle loro piste le carovane, avanzano nel deserto e vi si perdono;
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 le carovane di Tema guardano là, i viandanti di Saba sperano in essi:
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 ma rimangono delusi d'avere sperato, giunti fin là, ne restano confusi.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Così ora voi siete per me: vedete che faccio orrore e vi prende paura.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Vi ho detto forse: «Datemi qualcosa» o «dei vostri beni fatemi un regalo»
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 o «liberatemi dalle mani di un nemico» o «dalle mani dei violenti riscattatemi»?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Istruitemi e allora io tacerò, fatemi conoscere in che cosa ho sbagliato.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Che hanno di offensivo le giuste parole? Ma che cosa dimostra la prova che viene da voi?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Forse voi pensate a confutare parole, e come sparsi al vento stimate i detti di un disperato!
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Anche sull'orfano gettereste la sorte e a un vostro amico scavereste la fossa.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Ma ora degnatevi di volgervi verso di me: davanti a voi non mentirò.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Su, ricredetevi: non siate ingiusti! Ricredetevi; la mia giustizia è ancora qui!
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 C'è forse iniquità sulla mia lingua o il mio palato non distingue più le sventure?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?