< Giobbe 34 >
2 Ascoltate, saggi, le mie parole e voi, sapienti, porgetemi l'orecchio,
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 Perché l'orecchio distingue le parole, come il palato assapora i cibi.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 Esploriamo noi ciò che è giusto, indaghiamo fra di noi quale sia il bene:
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 poiché Giobbe ha detto: «Io son giusto, ma Dio mi ha tolto il mio diritto;
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 contro il mio diritto passo per menzognero, inguaribile è la mia piaga benché senza colpa».
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 Chi è come Giobbe che beve, come l'acqua, l'insulto,
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 che fa la strada in compagnia dei malfattori, andando con uomini iniqui?
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 Poiché egli ha detto: «Non giova all'uomo essere in buona grazia con Dio».
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 Perciò ascoltatemi, uomini di senno: lungi da Dio l'iniquità e dall'Onnipotente l'ingiustizia!
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 Poiché egli ripaga l'uomo secondo il suo operato e fa trovare ad ognuno secondo la sua condotta.
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 In verità, Dio non agisce da ingiusto e l'Onnipotente non sovverte il diritto!
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 Chi mai gli ha affidato la terra e chi ha disposto il mondo intero?
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 Se egli richiamasse il suo spirito a sè e a sé ritraesse il suo soffio,
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 ogni carne morirebbe all'istante e l'uomo ritornerebbe in polvere.
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 Se hai intelletto, ascolta bene questo, porgi l'orecchio al suono delle mie parole.
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 Può mai governare chi odia il diritto? E tu osi condannare il Gran Giusto?
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 lui che dice ad un re: «Iniquo!» e ai principi: «Malvagi!»,
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 lui che non usa parzialità con i potenti e non preferisce al povero il ricco, perché tutti costoro sono opera delle sue mani?
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 In un istante muoiono e nel cuore della notte sono colpiti i potenti e periscono; e senza sforzo rimuove i tiranni,
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 poiché egli tiene gli occhi sulla condotta dell'uomo e vede tutti i suoi passi.
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 Non vi è tenebra, non densa oscurità, dove possano nascondersi i malfattori.
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 Poiché non si pone all'uomo un termine per comparire davanti a Dio in giudizio:
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 egli fiacca i potenti, senza fare inchieste, e colloca altri al loro posto.
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 Poiché conosce le loro opere, li travolge nella notte e sono schiacciati;
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 come malvagi li percuote, li colpisce alla vista di tutti;
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 perché si sono allontanati da lui e di tutte le sue vie non si sono curati,
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 sì da far giungere fino a lui il grido dell'oppresso e fargli udire il lamento dei poveri.
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 Se egli tace, chi lo può condannare? Se vela la faccia, chi lo può vedere? Ma sulle nazioni e sugli individui egli veglia,
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 perché non regni un uomo perverso, perché il popolo non abbia inciampi.
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 Si può dunque dire a Dio: «Porto la pena, senza aver fatto il male;
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 se ho peccato, mostramelo; se ho commesso l'iniquità, non lo farò più»?
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 Forse, secondo le tue idee dovrebbe ricompensare, perché tu rifiuti il suo giudizio? Poiché tu devi scegliere, non io, dì, dunque, quello che sai.
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 Gli uomini di senno mi diranno con l'uomo saggio che mi ascolta:
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 «Giobbe non parla con sapienza e le sue parole sono prive di senno».
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 Bene, Giobbe sia esaminato fino in fondo, per le sue risposte da uomo empio,
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 perché aggiunge al suo peccato la rivolta, in mezzo a noi batte le mani e moltiplica le parole contro Dio.
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”