< Giobbe 16 >

1 Allora rispose:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Ne ho udite gia molte di simili cose! Siete tutti consolatori molesti.
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Non avran termine le parole campate in aria? O che cosa ti spinge a rispondere così?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 Anch'io sarei capace di parlare come voi, se voi foste al mio posto: vi affogherei con parole e scuoterei il mio capo su di voi.
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 Vi conforterei con la bocca e il tremito delle mie labbra cesserebbe.
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 Ma se parlo, non viene impedito il mio dolore; se taccio, che cosa lo allontana da me?
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 Ora però egli m'ha spossato, fiaccato, tutto il mio vicinato mi è addosso;
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 si è costituito testimone ed è insorto contro di me: il mio calunniatore mi accusa in faccia.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 La sua collera mi dilania e mi perseguita; digrigna i denti contro di me, il mio nemico su di me aguzza gli occhi.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 Spalancano la bocca contro di me, mi schiaffeggiano con insulti, insieme si alleano contro di me.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 Dio mi consegna come preda all'empio, e mi getta nelle mani dei malvagi.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 Me ne stavo tranquillo ed egli mi ha rovinato, mi ha afferrato per il collo e mi ha stritolato; ha fatto di me il suo bersaglio.
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 I suoi arcieri mi circondano; mi trafigge i fianchi senza pietà, versa a terra il mio fiele,
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 mi apre ferita su ferita, mi si avventa contro come un guerriero.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 Ho cucito un sacco sulla mia pelle e ho prostrato la fronte nella polvere.
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 La mia faccia è rossa per il pianto e sulle mie palpebre v'è una fitta oscurità.
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 Non c'è violenza nelle mie mani e pura è stata la mia preghiera.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 O terra, non coprire il mio sangue e non abbia sosta il mio grido!
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 Ma ecco, fin d'ora il mio testimone è nei cieli, il mio mallevadore è lassù;
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 miei avvocati presso Dio sono i miei lamenti, mentre davanti a lui sparge lacrime il mio occhio,
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 perché difenda l'uomo davanti a Dio, come un mortale fa con un suo amico;
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 poiché passano i miei anni contati e io me ne vado per una via senza ritorno.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

< Giobbe 16 >