< Warumi 2 >
1 Kululo wimugila uiteteli uewe ni wiapeza iantu ulamulwa, kunsoko ayo niwialamuila niangiza uewe niaza peza iantu uulamulya wituma nkani zizo zizo.
Kwa hiyo hauna udhuru, wewe uhukumuye, kwa maana katika yale uhukumuyo mwingine wajitia hatiani mwenyewe. Kwa maana wewe uhukumuye unafanya mambo yale yale.
2 Ingi kulingila kina ulamulwa wang'wi Tunda ingi watai kuantu niituma inkani anga nianso.
Lakini twajua kwamba hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao mambo kama hayo.
3 Kululo uewe siga ili, ue nualamula ao niituma inkani nianso, kunu nuewe wituma zizozizo, kulunge uziza uutiga ne ulamulwa wang'wi Tunda?
Lakini wewe tafakari hili, wewe ambaye unahukumu wale wanaotenda mambo hayo ingawa nawe unafanya mambo yayo hayo. Je utaepuka hukumu ya Mungu?
4 Ang'wi usigile inino kuuza nua udu wa uza wakwe, kutiya upilya wakwe nu gimya wakwe? Singa ulingile kina uuza wakwe. Unonee kuumanyisa uungami nuamunkolo.
Au unafikiri kidogo sana juu ya wingi wa wema wake, kuchelewa kwa adhabu yake, na uvumilivu wake? Je, hujui kwamba wema wake unapaswa kukuelekeza katika toba?
5 Kunsoko aukaku wako ninkolo ako ningila uugombi ukiikilya uewe imbago nia ubi kuluhiku ulo nula ubi. Ingi uluhiku ulo nulaukunukulwa pa ulamuli wa tai nuang'wi Tunda.
Bali kwa kadiri ya ugumu wako na kwa moyo wako usio na toba wajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu kwa siku ile ya ghadhabu, yaani, siku ile ya ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu.
6 Nuanso uzepumya ukinya mulimo anga intendo yako naiwituma muunkumbigulu.
Yeye atamlipa kila mtu kipimo sawa na matendo yake:
7 Awa naituma iza intendo yao yaapeza lukumo luza ikolyo nukuhita kugazika. Uzeapa utemi wamahiku ihi. (aiōnios )
kwa wale ambao kwa uthabiti wa matendo mema wametafuta sifa, heshima na kutokuharibika, atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
8 Kululo ao niagila itai, nishaigombi itai ilowa uubi ulaki wang'wi Tunda upembilye.
Lakini kwa wale ambao ni wabinafsi, wasioitii kweli bali hutii dhuluma, ghadhabu na hasira kali itakuja.
9 Itunda ukuleta uubi nuagi kumuntu naiwitumile imilandu, kung'wa Muyahudi hanza nukung'wa Muyunani.
Mungu ataleta dhiki na shida juu ya kila nafsi ya binadamu aliyefanya uovu, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
10 Kululo lukumo nuluza, ikulyo nuupolo ukiza kumuntu nuitumile nimaza, kumu uyahudi hanzo nu kumuyunani.
Lakini sifa, heshima na amani itakuja kwa kila mtu atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
11 Kunsoko kutile anga wiguniili kung'wi Tunda.
Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
12 Kunsoko anga naiauiye bila ulamulwa akulimila singa azeakoli mulamulwa anga wawa niidu naiauiye niakite uulamulwa azizapegwa uulamulwa tai.
Kwa maana kama vile wengi waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na kama vile wengi waliokosa kulingana na sheria watahukumiwa kwa sheria.
13 Kunsoko singa iji aunonelya nuatai pantongeela ang'wi Tunda. ingi ao niituma unonelya niazepegwa itai.
Maana si wasikiaji wa sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
14 Kunsoko iantu amunkumbigulu, niagila unoneelya, akituma kunkani ya unoneelya, nianso aile unoneelya ankolo yao hangi nianso agila anga unoneelya.
Kwa maana watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanafanya kwa asili mambo ya sheria, wao, wamekuwa sheria kwa nafsi zao, ingawa wao hawana sheria.
15 Kua ili akulagiila intendo niitakiwe munoneelya wa nkani wandikilwe munkolo yao, hangi inkolo yao yeenda singa, nimasigo ao akenda asemela ienso,
Kwa hili wanaonesha kwamba matendo yanayohitajika kwa mujibu wa sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia zinawashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama huwashitaki au huwalinda wao wenyewe
16 hangi Itunda ayo azipumula mumahiku ni Tunda uzeitamula inkunkuni ya antu ihi kunsoko alukani lakwe naigula nulang'wa Yesu Kilisto.
na pia kwa Mungu. Haya yatatokea katika siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu wote, sawasawa na injili yangu, kwa njia ya Yesu Kristo.
17 Kulunge gwa weendi itanga wi Myahudi, naiwikie muzeepilya wawa nkani lumbiilya kikulya kung'wi Tunda.
Tuseme kwamba unajiita mwenyewe Myahudi, aliyekaa katika sheria, shangilia kwa kujisifu katika Mungu,
18 Ulinge ulowa wakwe, nukusiga inkani nishayimpyani ni ninyanso, anga walagiligwa nu nanelya wa nkani.
yajue mapenzi yake, na kupima mambo ambayo yanatofautiana nayo, baada ya kuagizwa na sheria.
19 Kulunge kina ueweukite ugimya uewe hangi wimutongee wa apoku, wilu mulikua ao nikuli mukiti.
Na tuseme kwamba una ujasiri kwamba wewe mwenyewe ni kiongozi wa kipofu, mwanga kwa wale walio gizani,
20 Mumanyisi wa apungu, mmanyisi wa ang'enya hangi utite munonelya nua uhugu nua tai.
msahihishaji wa wajinga, mwalimu wa watoto, na kwamba unayo katika sheria jinsi ya elimu na kweli.
21 Uewe gwa nuimutanantilya numungiza, uewe sha wimanyisa nuewe? Ue nuitanantya kuleka kia uewe wia ne?
Wewe basi, uhubiriye mwingine, je, hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kutokuiba, je wewe huiba?
22 Ue nuiluga leka kugoolya, wigoolya ne?
Wewe usemae usizini, je unazini? Wewe uchukiaye sanamu, je unaiba hekaluni?
23 Ue nuikulya milago shawimuhumya ni Tunda iminyala kubunanga ilago?
Wewe ujisifuye katika sheria, je haumfedheheshi Mungu katika kuvunja sheria?
24 Kunsoko ilina lang'wa Itunda likuhumigwa minyala kuantu nishanga ahuie kunsoko anyu, anga naiyandikilwe.
Kwa maana “jina la Mungu linafedheheshwa kati ya watu wa mataifa kwa sababu yenu,” kama ilivyoandikwa.
25 Kunsoko kutalwa kukidamu ni ka tai inonea anga wizugombile kilago, kuhulo uewe ang'wi wimubunangi ilago kutwala kukidamu kung'wako izeze nakanda.
Kwa maana Kutahiriwa kweli kwafaa kama ukitii sheria, lakini kama wewe ni mkiukaji wa sheria, kutahiriwa kwako kunakuwa kutokutahiriwa.
26 Ang'wi umuntu nisinga utawi kukidamu ulongolekile kukie milago. Kuhita kutwalwa kukila kitalakwe ukutula kina singa utawe kukidamu?
Basi, ikiwa, mtu asiyetahiriwa anaendelea kushika matakwa ya sheria, je kutokutahiriwa kwake hakutachukuliwa kana kwamba ametahiriwa?
27 Nuyu nisinga utwawe kukidamu puma ung'wandyo, singa ukutula lamula anga akondyo kuamba ilago? Iye ingi kunsoko akoli naandikilwe kilago kunu akili mubunangi wi lago.
Na yeye asiyetahiriwa kwa asili hatakuhukumu kama akitimiza sheria? Hii ni kwa sababu una maandiko yaliyoandikwa na tohara pia lakini bado u mkiukaji wa sheria!
28 Kunsoko uyu singa Muyahudi nukoli muhali akunzi, hangi kukidamu singa uko nia koli kunzi du kimuiili.
Kwa maana yeye si Myahudi aliye kwa hali ya nje; wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje tu katika mwili.
29 Kululo nuanso Myahudi nuamkati ni lago nila munkolo mung'wang'waung'welu, singa miandiko. Ulukumo la muntu anga uyu shalipumiila anga kuantu lipumaa kung'wi Tunda.
Lakini yeye ni Myahudi aliye kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko. Sifa ya mtu wa namna hiyo haitokani na watu bali yatoka kwa Mungu.