< Bilangan 31 >

1 TUHAN berkata kepada Musa,
Bwana akamwambia Mose,
2 "Lakukanlah pembalasan kepada orang Midian karena apa yang sudah mereka perbuat terhadap bangsa Israel. Sesudah itu engkau akan mati."
“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
3 Maka Musa berkata kepada bangsa Israel, "Bersiap-siaplah untuk berperang; kamu harus menyerang orang Midian untuk melakukan hukuman TUHAN terhadap mereka.
Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
4 Dari setiap suku bangsa Israel, kamu harus menyiapkan seribu orang prajurit untuk maju berperang."
Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
5 Maka dipilihlah seribu orang dari setiap suku bangsa Israel, seluruhnya berjumlah dua belas ribu orang yang siap bertempur.
Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
6 Musa menyuruh mereka berperang bersama-sama dengan Pinehas anak Imam Eleazar. Pinehas membawa benda-benda suci dan trompet-trompet untuk memberi tanda-tanda.
Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
7 Sesuai dengan perintah TUHAN kepada Musa, orang Israel menyerang orang Midian dan membunuh semua orang laki-lakinya,
Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
8 termasuk lima raja Midian, yaitu Ewi, Rekem, Zur, Hur dan Reba. Bileam, anak Beor, juga dibunuh.
Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
9 Orang-orang Israel menawan para wanita dan anak-anak Midian, dan merampas segala hewan dan ternak, serta segala kekayaan mereka.
Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
10 Kota-kota dan perkemahan-perkemahan mereka pun dibakar.
Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
11 Setelah itu orang-orang Israel mengambil semua hasil rampasan itu, termasuk para tawanan dan hewan,
Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
12 lalu membawanya kepada Musa dan Imam Eleazar dan kepada seluruh umat Israel. Pada waktu itu mereka sedang berkemah di dataran Moab, di tepi Sungai Yordan, dekat kota Yerikho.
nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
13 Maka Musa, Imam Eleazar dan semua pemimpin lainnya dari umat Israel keluar dari perkemahan untuk menyambut tentara Israel.
Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
14 Musa memarahi para perwira, para kepala pasukan dan kepala laskar yang baru saja kembali dari pertempuran.
Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
15 Katanya kepada mereka, "Mengapa kamu membiarkan semua wanita itu hidup?
Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
16 Bukankah wanita-wanita itu yang menuruti nasihat Bileam, sehingga membujuk umat Israel di Peor untuk meninggalkan TUHAN? Dan itulah yang mendatangkan bencana atas umat TUHAN!
“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
17 Nah, sekarang bunuhlah setiap anak laki-laki dan setiap wanita yang bukan perawan lagi.
Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
18 Tetapi semua perempuan yang masih perawan boleh kamu ambil untukmu.
lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
19 Dan kamu semua yang telah membunuh orang atau menyentuh mayat harus tinggal di luar perkemahan selama tujuh hari. Pada hari yang ketiga dan yang ketujuh kamu dan semua wanita yang kamu tawan itu harus melakukan upacara penyucian diri.
“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
20 Setiap potong pakaian dan apa saja dari kulit, bulu kambing atau kayu, harus juga disucikan."
Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
21 Kemudian Imam Eleazar berkata kepada orang-orang yang baru kembali dari pertempuran itu, "Inilah peraturan-peraturan yang diberikan TUHAN kepada Musa.
Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
22 Segala sesuatu yang tahan api, seperti emas, perak, tembaga, besi, timah putih dan timah hitam, harus disucikan dengan melalukannya dalam api. Kemudian barang-barang itu harus disucikan juga dengan air upacara penyucian supaya tidak najis lagi. Semua benda lainnya yang tidak tahan api harus disucikan dengan air upacara penyucian.
Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
24 Pada hari yang ketujuh kamu harus mencuci pakaianmu, barulah kamu tidak najis lagi, dan boleh masuk ke dalam perkemahan."
Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
25 TUHAN berkata kepada Musa,
Bwana akamwambia Mose,
26 "Engkau dan Imam Eleazar, bersama-sama dengan para pemimpin lainnya dari umat Israel, harus menghitung semua hasil rampasan, termasuk para tawanan dan hewan.
“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
27 Hasil rampasan itu harus kamu bagi dua yang sama banyaknya; sebagian untuk para prajurit yang telah pergi berperang, dan sebagian lagi untuk umat selebihnya.
Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
28 Untuk pemberian khusus kepada Aku, TUHAN, dari bagian para prajurit itu harus kauambil satu dari setiap lima ratus--baik dari orang-orang tawanan, maupun dari sapi, keledai, domba dan kambing.
Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
29 Serahkanlah itu kepada Imam Eleazar sebagai persembahan khusus untuk Aku, TUHAN.
Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
30 Dari bagian yang diberikan kepada umat Israel, harus kauambil satu dari setiap lima puluh, baik dari orang-orang tawanan, maupun dari sapi, keledai, domba dan kambing. Serahkanlah semuanya itu kepada orang Lewi yang mengurus Kemah-Ku."
Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
31 Musa dan Imam Eleazar melakukan seperti yang diperintahkan TUHAN.
Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Selain yang sudah diambil para prajurit untuk mereka sendiri, hasil rampasan itu berjumlah: 675.000 ekor domba dan kambing, 72.000 ekor sapi, 61.000 ekor keledai dan 32.000 orang gadis perawan.
Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
ngʼombe 72,000,
punda 61,000,
na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
36 Separuh dari jumlah itu diberikan kepada para prajurit dengan perincian ini: 337.500 ekor domba dan kambing, dan dari jumlah itu 675 ekor untuk pemberian khusus bagi TUHAN; 36.000 ekor sapi, 72 ekor untuk pemberian khusus bagi TUHAN; 30.500 ekor keledai, 61 ekor untuk pemberian khusus bagi TUHAN; 16.000 orang gadis perawan, 32 orang untuk pemberian khusus bagi TUHAN.
Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
41 Lalu Musa menyerahkan pemberian khusus itu kepada Imam Eleazar untuk persembahan bagi TUHAN, seperti yang diperintahkan TUHAN.
Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
42 Bagian untuk rakyat sama banyaknya dengan bagian untuk prajurit: 337.500 ekor domba dan kambing, 36.000 ekor sapi, 30.500 ekor keledai, dan 16.000 orang gadis perawan.
Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
ngʼombe 36,000,
punda 30,500,
na wanadamu 16,000.
47 Seperti yang diperintahkan TUHAN, Musa mengambil satu dari setiap lima puluh orang tawanan dan hewan, lalu menyerahkannya kepada orang-orang Lewi yang bertugas di Kemah TUHAN.
Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
48 Kemudian para perwira yang telah memimpin tentara Israel, menghadap Musa
Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
49 dan melaporkan, "Tuan, kami sudah menghitung para prajurit bawahan kami. Ternyata jumlah mereka lengkap, tak seorang pun yang hilang.
na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
50 Sebab itu kami membawa perhiasan-perhiasan emas, gelang tangan, gelang kaki, cincin, anting-anting dan kalung yang telah diambil oleh masing-masing. Semua ini kami serahkan kepada TUHAN sebagai persembahan kami, supaya Ia tetap melindungi kami."
Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
51 Lalu Musa dan Imam Eleazar menerima emas itu, semuanya dalam bentuk perhiasan.
Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
52 Persembahan para perwira itu beratnya hampir dua ratus kilogram.
Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
53 Tetapi prajurit-prajurit itu masing-masing telah mengambil hasil rampasan itu bagi mereka sendiri.
Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
54 Maka Musa dan Imam Eleazar membawa emas itu ke Kemah TUHAN supaya TUHAN melindungi bangsa Israel.
Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

< Bilangan 31 >