< 1 Tawarikh 29 >

1 Lalu berkatalah Raja Daud kepada semua orang yang berkumpul di situ, "Dari semua putraku, Salomolah yang dipilih Allah. Tetapi ia masih sangat muda dan kurang pengalaman, sedangkan pekerjaan ini sangat besar. Lagipula yang akan dibangun itu bukan istana untuk manusia, melainkan rumah untuk TUHAN Allah.
Ndipo Mfalme Daudi akaliambia kusanyiko lote: “Mwanangu Solomoni, yeye ambaye Mungu amemchagua, ni kijana mdogo na asiye na uzoefu. Kazi hii ni kubwa, kwa sababu Hekalu hili la fahari si kwa ajili ya mwanadamu bali ni kwa ajili ya Bwana.
2 Bahan-bahan untuk rumah itu beserta perabotnya sudah kusiapkan dengan segala kemampuanku. Aku telah menyediakan emas, perak, perunggu, besi, kayu, batu-batu berharga dan batu-batu permata, batu-batu beraneka warna untuk hiasan-hiasan dan sangat banyak batu pualam.
Kwa uwezo wangu wote nimetenga mali kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu: dhahabu kwa kazi za dhahabu, fedha kwa ajili ya fedha, shaba kwa kazi za shaba, chuma kwa kazi za chuma na miti kwa kazi za miti, vivyo hivyo vito vya shohamu kwa ajili ya kutia kwenye vijalizo, almasi, mawe ya rangi mbalimbali, aina zote za vito vya thamani na marmar; yote haya kwa wingi mno.
3 Bahkan karena cintaku kepada Rumah Allahku itu aku telah menyerahkan juga perak dan emas dari harta milikku sendiri:
Zaidi ya hayo, kwa kujitolea kwangu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, sasa ninatoa hazina zangu mwenyewe za dhahabu na fedha kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, zaidi ya mali niliyotoa kwa ajili ya Hekalu hili takatifu:
4 emas terbaik 100 ton lebih, dan perak murni kurang lebih 240 ton untuk melapisi dinding Rumah TUHAN, dan untuk benda-benda yang harus dikerjakan oleh para tenaga ahli. Nah, sekarang siapa lagi mau memberikan persembahannya kepada TUHAN dengan senang hati?"
talanta 3,000 za dhahabu (dhahabu ya Ofiri) na talanta 7,000 za fedha safi iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za Hekalu,
5
kwa kazi ya dhahabu na kazi ya fedha na kwa kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi, ni nani anayependa kujitoa kwa Bwana leo?”
6 Maka para kepala kaum, kepala suku, para perwira dan penanggung jawab harta milik raja menyatakan bahwa mereka ingin juga menyumbang.
Ndipo viongozi wa jamaa, maafisa wa kabila za Israeli, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, pamoja na maafisa waliokuwa wasimamizi wa kazi za mfalme wakatoa kwa hiari yao.
7 Lalu mereka pun memberikan yang berikut ini untuk pembangunan Rumah TUHAN itu: emas 170 ton lebih, perak 340 ton lebih, perunggu hampir 620 ton, dan besi 3.400 ton lebih.
Wakatoa kwa ajili ya kazi ya Hekalu la Mungu talanta 5,000 na darkoni 10,000 za dhahabu, talanta 10,000 za fedha, talanta 18,000 za shaba na talanta 100,000 za chuma.
8 Orang-orang yang memiliki batu-batu permata menyerahkannya kepada Yehiel untuk dimasukkan ke dalam kas Rumah TUHAN. (Yehiel adalah seorang Lewi dari kaum Gerson.)
Kila mmoja aliyekuwa na vito vya thamani akavitoa katika hazina ya Hekalu la Bwana chini ya uangalizi wa Yehieli Mgershoni.
9 Rakyat memberi dengan rela hati kepada TUHAN dan mereka gembira karena telah banyak yang mereka persembahkan. Raja Daud juga gembira sekali.
Watu wakafurahi kwa sababu ya itikio la hiari la viongozi wao, kwa kuwa walikuwa wametoa kwa hiari na kwa moyo wote kwa Bwana. Mfalme Daudi pia akafurahi sana.
10 Di hadapan orang banyak itu Raja Daud memuji TUHAN. Ia berkata, "Ya TUHAN Allah yang disembah Yakub leluhur kami, terpujilah Engkau untuk selama-lamanya!
Daudi akamhimidi Bwana mbele ya kusanyiko lote, akisema: “Uhimidiwe wewe, Ee Bwana, Mungu wa Israeli baba yetu, tangu milele hata milele.
11 Engkau sungguh besar, dan berkuasa. Engkau mulia, jaya dan agung. Segala sesuatu di langit dan di bumi adalah milik-Mu. Engkau raja agung, penguasa atas segalanya.
Ukuu na uweza, ni vyako, Ee Bwana, na utukufu na enzi na uzuri, kwa kuwa kila kilichoko mbinguni na duniani ni chako wewe. Ee Bwana, ufalme ni wako; umetukuzwa kuwa mkuu juu ya yote.
12 Semua kekayaan dan kemakmuran berasal daripada-Mu; segala sesuatu Engkau kuasai dengan kekuatan dan kedaulatan-Mu; Engkau berkuasa membuat siapa saja menjadi orang besar dan kuat.
Utajiri na heshima vyatoka kwako; wewe ndiwe utawalaye vitu vyote. Mikononi mwako kuna nguvu na uweza ili kuinua na kuwapa wote nguvu,
13 Sekarang, ya Allah kami, kami ucapkan syukur kepada-Mu, dan kami memuji nama-Mu yang agung.
Sasa, Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu Jina lako tukufu.
14 Aku dan rakyatku ini sesungguhnya tak dapat memberikan apa-apa kepada-Mu, karena segalanya adalah pemberian-Mu dan apa yang kami berikan ini adalah kepunyaan-Mu juga.
“Lakini mimi ni nani, nao watu wangu ni nani, hata tuweze kukutolea kwa ukarimu namna hii? Vitu vyote vyatoka kwako, nasi tumekutolea tu vile vitokavyo mkononi mwako.
15 Engkau tahu, ya TUHAN, bahwa seperti para leluhur kami, kami pun menjalani hidup ini sebagai pendatang dan orang asing. Hidup kami seperti bayangan yang berlalu, dan kami tidak bisa luput dari kematian.
Sisi ni wageni na wapitaji machoni pako, kama walivyokuwa baba zetu wote. Siku zetu duniani ni kama kivuli, bila tumaini.
16 Ya TUHAN, Allah kami, semua barang berharga ini kami kumpulkan di sini untuk mendirikan sebuah rumah bagi-Mu supaya kami dapat menghormati nama-Mu yang suci. Tetapi semuanya itu kami terima daripada-Mu sendiri dan adalah kepunyaan-Mu juga.
Ee Bwana Mungu wetu, kwa wingi wote huu ambao tumekutolea kwa kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina lako Takatifu, vimetoka mkononi mwako, navyo vyote ni mali yako.
17 Aku tahu Engkau menguji hati setiap orang dan Engkau menyukai orang yang murni hatinya. Dengan tulus ikhlas dan senang hati kupersembahkan semuanya ini kepada-Mu. Aku telah menyaksikan bagaimana umat-Mu yang berkumpul di sini membawa persembahan mereka kepada-Mu dengan senang hati.
Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe huujaribu moyo na unapendezwa na unyofu. Vitu hivi vyote nimetoa kwa hiari na kwa moyo mnyofu. Nami sasa nimeona kwa furaha jinsi watu wako walioko hapa kwa hiari yao walivyokutolea wewe.
18 Ya TUHAN Allah, yang disembah oleh Abraham, Ishak dan Yakub, leluhur kami, kiranya Engkau menjaga supaya umat-Mu tetap mencintai Engkau seperti sekarang ini dan tolonglah supaya mereka selamanya setia kepada-Mu.
Ee Bwana, Mungu wa baba zetu Abrahamu, Isaki na Israeli, weka shauku hii ndani ya mioyo ya watu wako daima na uifanye mioyo yao iwe na uaminifu kwako.
19 Berikanlah kepada Salomo, putraku, keinginan yang sungguh-sungguh untuk menuruti semua perintah-Mu dan untuk membangun rumah ibadat itu yang persiapannya sudah kulaksanakan."
Nawe umpe mwanangu Solomoni kujitolea kwako kwa moyo wote ili kuzishika amri zako, masharti yako, maagizo yako na kufanya kila kitu ili kujenga Hekalu hili la fahari ambalo kwa ajili yake nimetoa.”
20 Sesudah berdoa demikian, Daud berkata kepada orang banyak yang berkumpul di situ, "Pujilah TUHAN Allahmu!" Maka semua orang itu memuji-muji TUHAN, Allah yang disembah leluhur mereka. Lalu mereka sujud untuk menghormati TUHAN dan raja.
Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote, “Mhimidini Bwana Mungu wenu.” Hivyo wote wakamhimidi Bwana, Mungu wa baba zao. Wakasujudu na kuanguka kifudifudi mbele za Bwana na mfalme.
21 Hari berikutnya mereka menyembelih hewan untuk dipersembahkan sebagai kurban kepada TUHAN, lalu dibagikan kepada seluruh rakyat. Selain itu ada 1.000 sapi jantan, 1.000 domba jantan dan 1.000 domba muda yang disembelih dan dibakar utuh di atas mezbah. Mereka juga mempersembahkan anggur yang diwajibkan untuk kurban-kurban itu.
Siku ya pili yake wakamtolea Bwana dhabihu na sadaka za kuteketezwa: mafahali 1,000, kondoo dume 1,000 na wana-kondoo dume 1,000, pamoja na sadaka za kinywaji na sadaka nyingine nyingi sana kwa ajili ya Israeli.
22 Hari itu mereka makan minum dengan gembira di hadapan TUHAN. Lalu untuk kedua kalinya mereka memproklamasikan Salomo sebagai raja. Atas nama TUHAN, mereka meresmikan dia menjadi raja mereka dan Zadok menjadi imam.
Wakala na kunywa kwa furaha kubwa mbele za Bwana siku ile. Wakamtawaza Solomoni mwana wa Daudi mara ya pili kuwa mfalme, wakamtia mafuta kwa ajili ya Bwana ili awe mfalme na Sadoki kuwa kuhani.
23 Maka sebagai pengganti Daud ayahnya, Salomo naik takhta yang telah ditetapkan oleh TUHAN. Ia raja yang sukses dan disegani oleh seluruh bangsa Israel.
Solomoni akaketi kwenye kiti cha enzi cha Bwana kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yake. Akafanikiwa sana na Israeli wote wakamtii.
24 Semua pejabat pemerintahan dan militer sampai kepada putra-putra Daud yang lain pun mengakui kekuasaan Salomo sebagai raja.
Maafisa wote na mashujaa, pamoja na wana wote wa Daudi, wakaahidi kumtii Mfalme Solomoni.
25 TUHAN membuat seluruh rakyat mengagumi Raja Salomo dan menjadikannya raja yang lebih hebat dari raja mana pun juga yang pernah memerintah Israel.
Bwana akamtukuza sana Solomoni mbele ya Israeli wote na kumvika fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli kabla yake aliwahi kuwa nayo.
26 Daud anak Isai memerintah seluruh Israel
Daudi mwana wa Yese alikuwa mfalme wa Israeli yote.
27 empat puluh tahun lamanya. Di Hebron ia memerintah selama 7 tahun dan di Yerusalem selama 33 tahun.
Alitawala Israeli kwa miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
28 Ia kaya dan terhormat dan meninggal pada usia lanjut. Salomo putranya menjadi raja menggantikan dia.
Daudi akafa akiwa mzee mwenye umri mwema, akiwa ameshiba siku, utajiri na heshima. Naye Solomoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
29 Riwayat hidup Raja Daud dari mula sampai akhir telah dicatat dalam buku Nabi Samuel, Nabi Natan dan Nabi Gad.
Kuhusu matukio ya utawala wa Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kumbukumbu za mwonaji Samweli, na kumbukumbu za nabii Nathani na kumbukumbu za mwonaji Gadi,
30 Dalam buku itu diceritakan tentang pemerintahannya, kekuasaannya dan segala yang terjadi atas dirinya, atas Israel dan kerajaan-kerajaan di sekitar Israel.
pamoja na habari zote za utawala wake, nguvu zake na matukio yaliyompata yeye, na Israeli, na falme za nchi nyingine zote.

< 1 Tawarikh 29 >