< Ezekiel 25 >

1 Kalpasanna, immay kaniak ti sao ni Yahweh a kunana,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 ”Anak ti tao, isangom ti rupam kadagiti tattao ti Ammon ket agipadtoka maibusor kadakuada.
“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Waamoni utabiri dhidi yao.
3 Ibagam kadagiti tattao ti Ammon, ‘Denggenyo ti sao ti Apo a ni Yahweh. Kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh: Kinunayo, “Aha!” maibusor iti santuariok idi natulawan daytoy, ken maibusor iti daga ti Israel idi nagbalin a langalang daytoy, ken maibusor iti balay ti Juda idi naipanawda a kas balud.
Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana Mwenyezi. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulisema, “Aha!” juu ya mahali pangu patakatifu palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli ilipoangamizwa, na juu ya watu wa Yuda walipokwenda uhamishoni,
4 Ngarud, dumngegkayo! Iyawatkayon kadagiti tattao iti daya a kas sanikuada; mangiyaramiddanto iti kampoda a maibusor kadakayo ken iyaramidda dagiti toldada iti ayanyo. Kanendanto dagiti bunga ti mulayo, ken inumendanto dagiti gatasyo!
kwa hiyo nitawatia mikononi mwa watu wa mashariki mkawe mali yao. Watapiga kambi zao katikati yenu na kufanya makazi miongoni mwenu, watakula matunda yenu na kunywa maziwa yenu.
5 Ket pagbalinekto ti Rabba a maysa a pagpaaraban kadagiti kamelio ken pagpaaraban kadagiti arban ti talon dagiti tattao nga Ammon, isu a maammoanyonto a Siak ni Yahweh!
Nitaufanya mji wa Raba kuwa malisho ya ngamia na Amoni kuwa mahali pa kondoo pa kupumzikia. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
6 Ta kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh: Intipatyo dagiti imayo ken intabbugayo dagiti sakayo, ken nagragrag-okayo kadagiti amin a pananglalaisyo iti daga ti Israel.
Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa kuwa umepiga makofi yako na kufanya kishindo kwa miguu, mkifurahia kwa mioyo yenu miovu juu ya yale mabaya yaliyoipata nchi ya Israeli,
7 Isu a dumngegkayo! Isipatkonto kadakayo ti imak ken itedkayto a kas samsam kadagiti nasion. Isinakayto kadagiti tattao ken pukawenkayto kadagiti pagilian! Dadaelenkayto, ket maammoanyonto a Siak ni Yahweh!’
hivyo nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako na kukutoa kuwa nyara kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka kwenye mataifa na kukungʼoa katika nchi. Nitakuangamiza, nawe utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
8 Kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh, ‘Gapu ta ibagbaga ti Moab ken Seir, “Kitaenyo! Ti balay ti Juda ket kasla kadagiti dadduma a nasion!”
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu Moabu na Seiri wamesema, “Tazama, nyumba ya Yuda imekuwa kama mataifa mengine yote,”
9 Isu a dumngegkayo! Lukatakto dagiti beddeng iti Moab, manipud kadagiti siudadna nga ayan ti beddeng—ti kinangayed ti Bet Jesimot, Baal Meon ken Kariatim—
kwa hiyo nitaiondoa ile miji iliyo kando ya Moabu, kuanzia miji iliyoko mipakani, yaani: Beth-Yeshimothi, Baal-Meoni na Kiriathaimu, iliyo utukufu wa nchi hiyo.
10 kadagiti tattao iti daya a siguden a bumusbusor kadagiti tattao ti Ammon. Iyawatkonto ida a kasla maysa a sanikua tapno dagiti tattao ti Ammon ket saanton a malagip pay kadagiti nasion.
Nitaitia Moabu pamoja na Waamoni mikononi mwa watu wa Mashariki kuwa milki yao, ili kwamba Waamoni wasikumbukwe miongoni mwa mataifa,
11 Isu a kedngakto dagiti taga-Moab, ket maammoandanto a Siak ni Yahweh!’
nami nitatoa adhabu kwa Moabu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
12 Kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh, ‘Binales dagiti taga-Edom ti balay ti Juda ket nagbiddutda iti panangaramidda iti kasta.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu Edomu ulilipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na kukosa sana kwa kufanya hivyo,
13 Isu a kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh: Isipatkonto ti imak iti Edom ken dadaelek ti amin a tao ken ayup sadiay. Pagbalinekto ida a nadadael, nabaybay-an a lugar, manipud Teman agingga iti Dedan. Mapasagdanto babaen iti kampilan!
kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuua watu wake na wanyama wao. Nitaufanya ukiwa, kuanzia Temani hadi Dedani wataanguka kwa upanga.
14 Iti kastoy a wagas, makaibalesakto iti Edom babaen iti ima dagiti tattaok nga Israelita, ket ipalak-amdanto iti Edom ti nalaus nga unget ken pungtotko! Isu a maammoandanto ti panagibalesko! —kastoy ti pakaammo ti Apo a ni Yahweh!’
Nitalipiza Edomu kisasi kwa mkono wa watu wangu Israeli, nao watawatendea Edomu sawasawa na hasira yangu na ghadhabu yangu, nao watakijua kisasi changu, asema Bwana Mwenyezi.’”
15 Kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh, ‘Nagibales dagiti Filisteo gapu iti nalaos a gurada ken inulit-ulitda a pinadpadas a dadaelen ti Juda.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu Wafilisti wamewalipiza kisasi kwa uovu wa mioyo yao na kwa uadui wa siku nyingi wakataka kuangamiza Yuda,
16 Isu a kastoy ti kuna ti Apo a ni Yahweh: Dumngegkayo! Iyunnatkonto ti imak kadagiti Filisteo, ken isinakto dagiti Kereteo ken dadaelek dagiti nabatbati nga adda kadagiti igid ti baybay!
kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ninakaribia kuunyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, nami nitawakatilia mbali Wakerethi na kuwaangamiza wale waliosalia katika pwani.
17 Ta balsekto ida iti nakaro babaen iti nakaro a panangdusak kadakuada, isu a maammoandanto a Siak ni Yahweh, inton balsek ida!”’
Nitalipiza kisasi kikubwa juu yao na kuwaadhibu katika ghadhabu yangu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapolipiza kisasi juu yao.’”

< Ezekiel 25 >