< I Samuel 3 >

1 Nagserbi ti ubing a ni Samuel kenni Yahweh babaen iti panangidalan ni Eli. Manmano ti sao ni Yahweh kadagidiay nga al-aldaw; awan unay ti sirmata maipanggep iti masakbayan.
Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.
2 Iti dayta a tiempo, idi ni Eli nga agkapsuten ti panagkitana a saan unayen a makakita, ket agid-idda iti bukodna a pagiddaan,
Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida.
3 Saan pay idi a naiddep ti pagsilawan ti Dios, ket ni Samuel, matmaturog iti balay ni Yahweh nga ayan ti lakasa ti tulag ti Dios.
Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
4 Inawagan ni Yahweh ni Samuel, a nagkuna, “Adtoyak.”
Kisha Bwana akamwita Samweli. Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
5 Timmaray ni Samuel iti ayan ni Eli, ket kinunana, “Immayak ta inayabannak.” Kinuna ni Eli, “Saanka nga inayaban; agsublika iti pagiddaam.” Isu a napan nagidda ni Samuel.
Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.
6 Immawag manen ni Yahweh, “Samuel.” Bimmangon manen ni Samuel ket napan kenni Eli ket kinunana, “Inayabannak isu nga adtoyak.” Simmungbat ni Eli, “Saanka nga inayaban, anakko; inka pay agidda.”
Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”
7 Ita, awan pay ti kapadasan ni Samuel kenni Yahweh, wenno awan pay pulos ti aniaman a mensahe a naipakita kenkuana manipud kenni Yahweh.
Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8 Inawagan manen ni Yahweh ni Samuel iti maikatlo a gundaway. Bimmangon manen ni Samuel ket napan kenni Eli ket kinunana, “Immayak ta inayabannak.” Ket naamiris ni Eli nga inawagan ni Yahweh ti ubing.
Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.” Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana.
9 Ket kinuna ni Eli kenni Samuel, “Mapanka agidda manen; no awagannaka manen, nasken nga ibagam, 'Agsaoka, O Yahweh, ta dumdumngeg ti adipenmo.”' Isu a napan nagidda manen ni Samuel iti pagid-iddaanna.
Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.
10 Immay ni Yahweh ket nagtakder; immawag a kas iti immuna, “Samuel, Samuel.” Ket kinuna ni Samuel, “Agsaoka, ta dumdumngeg ti adipenmo.”
Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!” Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
11 Kinuna ni Yahweh kenni Samuel, “Dumngegka, umadanin nga aramidek iti Israel ti banag nga uray la agkintayeg dagiti lapayag ti amin a makangngeg iti daytoy.
Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe.
12 Iti dayta nga aldaw, ipatungpalkonto kenni Eli dagiti amin nga imbagak maipanggep iti balayna, manipud iti rugi agingga iti pagpatinggaan.
Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
13 Imbagak kenkuana a dandanin nga ukomek a mammaminsan ti balayna gapu iti amin a basol nga ammona, gapu ta nangiyeg iti lunod dagiti annakna kadagiti bagbagida ket saanna ida nga inatipa.
Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia.
14 Gapu iti daytoy, insapatak iti balay ni Eli a saanto pulos a mapakawan dagiti basol ti balayna babaen iti daton wenno sagut.”
Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’”
15 Nagidda ni Samuel agingga iti bigat; kalpasanna, linukatanna dagiti ruangan ti balay ni Yahweh. Ngem mabuteng ni Samuel a mangibaga kenni Eli iti maipanggep iti sirmata.
Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono,
16 Ket inayaban ni Eli ni Samuel a kunana, “Samuel, anakko.” Kinuna ni Samuel, “Adtoyak.”
lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.” Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”
17 Kinuna ni Eli, “Ania ti imbagana kenka? Saanmo koma nga ilimed kaniak. Dusaennaka ti Dios, ken ad-adda pay koma no ilimedmo kaniak ti aniaman nga imbagana kenka.”
Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.”
18 Imbaga amin ni Samuel kenkuana; awan ti inlimedna kenkuana. Kinuna ni Eli, “Ni Yahweh daytoy. Aramidenna koma ti kasayaatan a maaramid.”
Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”
19 Dimmakkel ni Samuel, ket adda kenkuana ni Yahweh ket awan ti pimmalso kadagiti padtona.
Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini.
20 Ammo ti entero nga Israel manipud Dan agingga iti Beerseba a nadutokan ni Samuel nga agbalin a profeta ni Yahweh.
Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana.
21 Nagparang manen ni Yahweh idiay Silo, ta nagparang isuna a mismo kenni Samuel idiay Silo babaen iti saona.
Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.

< I Samuel 3 >