< I Samuel 28 >

1 Ket napasamak kadagidiay nga aldaw nga inummong dagiti Filisteo dagiti armadada para iti gubat tapno makirangetda iti Israel. Kinuna ni Akis kenni David, “Ipasiguradom a makikuyogka iti armadak a mapan rumaut, sika ken dagiti tattaom.”
Ikawa katika siku hizo Wafilisti walikusanya majeshi yao pamoja kwa ajili ya vita, wapigane na Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Ujue kwa hakika kwamba utakwenda nami ndani ya jeshi, wewe na watu wako.”
2 Kinuna ni David kenni Akis, “Maammoamto ngarud no ania ti kabaelan nga aramiden ti adipenmo.” Kinuna ni Akis kenni David, “Isu a sikanto ti mangsalaknib kaniak agingga a sibibiagak.”
Naye Daudi akamwambia Akishi, “Sasa utajua kile ambacho mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamwambia Daudi, “Basi sasa, nitakufanya uwe mlinzi wangu binafsi daima.”
3 Ita, natayen ni Samuel; nagladingit ti entero nga Israel ket intabonda isuna idiay Rama, iti bukodna nga ili. Ita, imparit ni Saul iti daga ti pannakiuman kadagiti natay wenno kadagiti espiritu.
Samweli alikuwa amefariki; Waisraeli wote walimwomboleza na kumzika huko Rama, katika mji wake mwenyewe. Wakati huo Sauli alikuwa amewafukuza kutoka nchini wote walioongea na wafu au pepo.
4 Naguummong dagiti Filisteo ket immayda nagkampo idiay Sunem; ket inummong ni Saul ti Israel ket nagkampoda iti Gilboa.
Wafilisti walijikusanya wao wenyewe wakaja na kuweka kambi huko Shunemu; na Sauli akawakusanya Israeli wote pamoja, na wakaweka kambi yao huko Gilboa.
5 Idi nakita ni Saul ti armada dagiti Filisteo, nagbuteng isuna ket kasta unay ti panagkibba-kibba ti barukongna.
Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, aliogopa na moyo wake ukatetemeka sana.
6 Idi nagkararag ni Saul kenni Yahweh tapno agpatulong, saan isuna a sinungbatan ni Yahweh—uray babaen kadagiti tagtagainep wenno babaen iti Urim wenno babaen kadagiti profeta.
Sauli alipomuomba BWANA kwa ajili ya msaada, BWANA hakumjibu - si kwa ndoto wala kwa Urimu, wala kwa manabii.
7 Ket kinuna ni Saul kadagiti adipenna, “Ibirokandak iti babai a makium-uman kadagiti natay tapno mapanak makiuman kenkuana.” Kinuna dagiti adipenna kenkuana, “Wen, adda maysa a babai idiay Endor a makium-uman kadagiti natay.”
Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, “Mnitafutie mwanamke ambaye anaweza kuongea na wafu, ili ni mwendee na kutafuta msaada wake.” Watumishi wake wakamwambia, “Tazama, yupo mwanamke huko Endori awezaye kuongea na wafu.”
8 Nanglimlimo ni Saul, nagarruat iti sabali a pagan-anay, ket napan a kaduana ti dua a lallaki; rabii a napanda iti ayan ti babai. Kinunana, “Makiumanka para kaniak, pangngaasim, babaen iti pannakisaritam kadagiti natay, awagam ti siasinoman nga inaganak.
Basi Sauli akajigeuza, akavaa nguo nyingine tofauti, akaondoka yeye pamoja na watu wawili; wakamwendea yule mwanamke wakati wa usiku. Akasema, “Nitabirie, nakuomba, kwa kuongea na wafu, na uniinulie yule nitakayekutajia.”
9 Kinuna ti babai kenkuana, “Saanmo aya nga ammmo ti inaramid ni Saul, no kasano ti panangiparitna iti daga iti pannakiuman kadagiti natay wenno kadagiti espiritu. Isu nga apay a kayatnak a palab-ogan, tapno ipapataynak?”
Yule mwanamke akamwambia, “Tazama, unajua alichofanya Sauli, jinsi alivyowafukuza kutoka katika nchi wanaoongea na wafu au mizimu. Basi kwa nini mnatega mtego kwa ajili ya uhai wangu, ili kuniua?”
10 Nagsapata ni Saul kenkuana iti nagan ni Yahweh a kinunana, “Iti nagan ni Yahweh nga adda iti agnanayon, awan ti pannusa a mapasamakto kenka gapu iti daytoy a banag.”
Sauli akamwapia kwa BWANA na kusema, “Kama BWANA aishivyo, hakuna adhabu utakayopata kutokana na jambo hili.”
11 Ket kinuna ti babai, “Siasino ngarud ti awagak para kenka?” Kinuna ni Saul, “Awagam ni Samuel para kaniak.”
Kisha yule mwanamke akasema, “Je, nikuinulie nani?” Sauli akasema, “Niinulie Samweli.”
12 Idi nakita ti babai ni Samuel, nagriaw isuna ket nagsao kenni Saul a kinunana, “Apay nga inallilawnak? Sika ni Saul.”
Yule mwanamke alipomwona Samweli, akalia kwa sauti kuu na kusema na Sauli, akisema, “Kwa nini umenidanganya? Maana wewe ni Sauli.”
13 Kinuna ti ari kenkuana, “Saanka nga agbuteng. Ania ti makitam?” Kinuna ti babai kenni Saul, “Makitkitak ti maysa a dios a rum-rummuar manipud iti daga.”
Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona kitu gani?” Yule mwanamke akamwambia Sauli, “Naona mungu akitoka katika nchi.” Akamuuliza mwanamke,
14 Kinunana kenkuana, “Ania ti langana?” Kinuna ti babai, “Maysa a lakay ti rum-rumuar; nakakagay iti atiddog.” Ammon ni Saul a dayta ni Samuel, ket nagrukob isuna iti daga a mangipakita iti panagraemna kenkuana.
“Je, anafanana na nani?” Mwanamke akajibu, “Mtu mzee anazuka; naye amevaa kanzu.” Sauli akafahamu kuwa huyo ni Samweli, naye Sauli akainamisha uso wake hadi chini akionesha heshima.
15 Kinuna ni Samuel kenni Saul, “Apay a sininganak ken inawagannak?” Simmungbat ni Saul, “Mariribokanak unay, ta gubgubatendak dagiti Filisteo, ken binaybay-annakon ti Dios ket saannakon a sungsungbatan, uray babaen kadagiti profeta, wenno babaen kadagiti tagtagainep. Isu nga inawaganka, tapno ipakaammom kaniak no ania ti aramidek.”
Samweli akamwambia Sauli, “Kwa nini umenisumbua na kuniinua juu?” Sauli akajibu, “Nimetaabika sana, maana Wafilisti wamepanga vita dhidi yangu, na Mungu ameniacha na hanipi majibu tena, si kwa manabii, wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita, ili unijulishe kile nitakachofanya.”
16 Kinuna ni Samuel, “Ania ngarud ti kiddawem kaniak, ita ta pinanawannakan ni Yahweh ken nagbalin isunan a kabusormo?
Samweli akasema, “Kwa kuwa BWANA amekuacha, basi unaniuliza nini, naye amekuwa adui yako?
17 Inaramid ni Yahweh kenka ti imbagana nga aramidenna. Inikkat ni Yahweh ti pagarian manipud kadagiti imam ket intedna daytoy iti sabali—kenni David.
BWANA amekutendea kile alichosema kuwa angekifanya. BWANA amerarua ufalme kutoka mkononi mwako na amempa ufalme mtu mwingine - amempa Daudi.
18 Gapu ta saanmo a tinungpal ti timek ni Yahweh ken saanmo nga impalak-am ti kasta unay a pungtotna kadagiti Amalekita, isu't gapuna nga inaramidna daytoy ita kenka.
Kwa sababu hukuitii sauti ya BWANA na hukutekeleza hasira yake kali juu ya Amaleki, kwa hiyo leo naye amefanya hili kwako.
19 Maysa pay, iyawatnakanto ni Yahweh ken ti Israel iti ima dagiti Filisteo. Inton bigat, sika ken dagiti annakmo ket maitiponto kaniak. Iyawatto met ni Yahweh ti armada ti Israel iti ima dagiti Filisteo.”
Zaidi ya hayo, BWANA atamweka Israeli pamoja na wewe katika mkono wa Wafilisti. Kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia ataliweka jeshi la Israeli katika mkono wa Wafilisti.”
20 Ket dagus a napasag ni Saul iti daga ket kasta unay ti butengna gapu kadagiti imbaga ni Samuel. Kimmapsut isuna, ta saan isuna a nangan iti nagmalmalem, uray iti dayta a nagpatnag.
Ndipo ghafla Sauli alianguka chini kifudifudi na aliogopa kwa sababu ya yale maneno ya Samweli. Aliishiwa nguvu mwilini mwake, kwa kuwa siku hiyo alikuwa hajala chakula, hata kwa usiku huo wote.
21 Immasideg ti babai kenni Saul ket nakitana a mariribokan unay isuna, kinunana kenkuana, “Kitaem, dinengngeg ti adipenmo a babai ti timekmo; impustak ti biagko ket dimngegak kadagiti sasao nga imbagam kaniak.
Ndipo yule mwanamke akaja kwa Sauli na akaona kwamba Sauli amepata shida, naye akamwambia, “Tazama, mjakazi wako ameisikiliza sauti yako; Nimeyaweka maisha yangu mkononi mwangu na nimeyasikiliza maneno uliyoniambia.
22 Ita ngarud, ipakpakaasik kenka, denggem met ti timek ti adipenmo a babai, ken ipalubosmo a mangidasarak iti bassit a taraon iti sangoanam. Manganka tapno pumigsaka iti panagawidmo.”
Hivyo basi, nakusihi, sikiliza pia sauti ya mjakazi wako, na uniruhusu nilete chakula kidogo mbele yako. Ule ili upate nguvu za kwenda kule uendako.”
23 Ngem nagkedked ni Saul ket kinunana, “Saanak a mangan.” Ngem impapilit dagiti adipen ni Saul, kasta met ti babai ket dimngeg isuna iti timekda. Timmakder ngarud manipud iti daga ket nagtugaw iti pagiddaan.
Lakini Sauli alikataa na kusema, “Sitakula.” Lakini watumishi wake, pamoja na yule mwanamke, wakamlazimisha hatimaye alisikiliza sauti zao. Hivyo aliinuka kutoka chini na kukaa kitandani.
24 Addaan ti babai iti napalukmeg a baka iti balayna; nagdardaras a nangparti iti daytoy; nangala iti arina, minasana daytoy, ket linutona daytoy a tinapay nga awan laokna a lebadurana.
Yule mwanamke alikuwa na ndama mnono hapo nyumbani; akafanya haraka na kumchinja; akachua unga, akaukanda, na akatengeneza mikate isiyotiwa chachu kwa unga huo.
25 Inyegna daytoy iti sangoanan ni Saul ken kadagiti adipenna, ket nanganda. Kalpasanna, nagrubbuatda ket pimmanawda iti dayta a rabii.
Akaileta mbele ya Sauli na watumishi wake, nao wakala. Baaadaye waliinuka na kuondoka usiku huo.

< I Samuel 28 >