< 1 इतिहास 6 >
1 लेवी के पुत्र: गेरशोन, कोहाथ और मेरारी.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2 कोहाथ के पुत्र: अमराम, इज़हार, हेब्रोन और उज्ज़िएल.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3 अमराम की संतान: अहरोन, मोशेह और मिरियम. अहरोन के पुत्र: नादाब, अबीहू, एलिएज़र और इथामार.
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4 एलिएज़र पिता था फिनिहास का, फिनिहास अबीशुआ का,
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5 अबीशुआ बुक्की का, बुक्की उज्जी का,
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6 उज्जी ज़ेराइयाह का, ज़ेराइयाह मेराइओथ का,
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7 मेराइओथ अमरियाह का, अमरियाह अहीतूब का,
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8 अहीतूब सादोक का सादोक अहीमाज़ का,
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9 अहीमाज़ अज़रियाह का, अज़रियाह योहानन का,
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10 योहानन अज़रियाह का पिता था. यह वही अज़रियाह था, जिसने येरूशलेम में शलोमोन द्वारा बनाए गए भवन में पौरोहितिक सेवा की थी.
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11 अज़रियाह अमरियाह का, अमरियाह अहीतूब का,
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12 अहीतूब सादोक का, सादोक शल्लूम का,
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13 शल्लूम हिलकियाह का, हिलकियाह अज़रियाह का,
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14 अज़रियाह सेराइयाह का, सेराइयाह यहोत्सादाक का,
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15 जब याहवेह ने नबूकदनेज्ज़र द्वारा यहूदिया और येरूशलेम को बंधुआई में भेजा, तब यहोत्सादाक भी बंधुआई में ले जाया गया:
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
16 लेवी के पुत्र: गेरशोम, कोहाथ और मेरारी.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17 गेरशोम के पुत्रों के ये नाम है: लिबनी और शिमेई.
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18 कोहाथ के पुत्र: अमराम, इज़हार, हेब्रोन और उज्ज़िएल.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19 मेरारी के पुत्र: माहली और मूशी. पिताओं के आधार पर लेवी वंशजों के कुल इस प्रकार है:
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20 गेरशोम के कुल: उसका पुत्र लिबनी, उसका पुत्र याहाथ, उसका पुत्र ज़िम्माह,
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21 उसका पुत्र योआह, उसका पुत्र इद्दो, उसका पुत्र ज़ेराह, उसका पुत्र येआथेराई.
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22 कोहाथ के पुत्र: उसका पुत्र अम्मीनादाब, उसका पुत्र कोराह, उसका पुत्र अस्सिर,
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23 उसका पुत्र एलकाना, उसका पुत्र एबीआसफ़, उसका पुत्र अस्सिर,
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24 उसका पुत्र ताहाथ, उसका पुत्र उरीएल, उज्जियाह उसका पुत्र, शाऊल उसका पुत्र.
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25 एलकाना के पुत्र ये थे: आमासाई, अहीमोथ,
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26 उसका पुत्र एकानाह, एलकाना के पुत्र थे ज़ोफ़ाई, उसका पुत्र नाहाथ,
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27 उसका पुत्र एलियाब, उसका पुत्र येरोहाम, उसका पुत्र एलकाना,
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28 शमुएल के पुत्र: उनका पहलौठा पुत्र योएल, दूसरा अबीयाह.
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29 मेरारी के पुत्र: माहली, उसका पुत्र लिबनी, उसका पुत्र शिमेई, उसका पुत्र उज्जाह,
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30 उसका पुत्र शिमिया, उसका पुत्र हाग्गियाह और उसका पुत्र असाइयाह.
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31 निम्न लिखित पुरुष वे हैं, जिन्हें दावीद ने याहवेह के भवन में संदूक की स्थापना के बाद आराधना में गाने की जवाबदारी सौंप रखी थी.
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32 ये येरूशलेम में शलोमोन द्वारा याहवेह का भवन बनाए जाने तक, मिलनवाले तंबू के सामने आराधना-संगीत के द्वारा सेवा करते थे. वे अपने पद के अनुसार ही यह सेवा किया करते थे.
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33 सेवा के लिए चुने गए उन व्यक्तियों और उनके पुत्रों के नाम इस प्रकार है: कोहाथ के पुत्रों में से: गायक, हेमान, जो योएल का पुत्र, शमुएल का पुत्र था,
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34 जो एलकाना का, जो येरोहाम का, जो एलिएल का, जो तौआह का,
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35 जो सूफ़ का, जो एलकाना का, जो माहाथ का, जो आमासाई का,
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36 जो एलकाना का, जो योएल का, जो अज़रियाह का, जो ज़ेफनियाह का,
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37 जो ताहाथ का, जो अस्सिर का, एबीआसफ़ का, जो कोराह का,
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38 जो इज़हार का, जो कोहाथ का, जो लेवी का, जो इस्राएल का पुत्र था.
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39 हेमान का सहकर्मी आसफ उसके दाएं पक्ष में खड़ा रहता था, जो वस्तुतः बेरेखियाह का पुत्र, शिमिया का पुत्र था.
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40 जो मिखाएल का पुत्र था, जो बासेइयाह का, जो मालखियाह का,
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41 जो एथनी का, जो ज़ेराह का, जो अदाइयाह का,
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42 जो एथन का, जो ज़िम्माह का, जो शिमेई का,
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43 जो याहाथ का, जो गेरशोम का, जो लेवी का पुत्र था.
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 उनके बाएं पक्ष में उनके संबंधी, मेरारी-वंशज खड़े हुआ करते थे: कीशी का पुत्र एथन, जो अबदी का, जो मल्लूख का,
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45 जो हशाबियाह का, जो अमाज़्याह का, जो हिलकियाह का,
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46 जो आमज़ी का, जो बानी का, जो शेमर का,
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47 जो माहली का, जो मूशी का, जो मेरारी का, जो लेवी का पुत्र था.
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 लेवी, उनके संबंधी, मिलनवाले तंबू और परमेश्वर के भवन संबंधी सेवा के लिए चुने गए थे.
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49 मगर अहरोन और उसके पुत्र वेदी पर होमबलि चढ़ाते और धूप वेदी पर धूप जलाते, परम पवित्र स्थान संबंधित कार्य और परमेश्वर के सेवक मोशेह के आदेश अनुसार इस्राएल के लिए प्रायश्चित किया करते थे.
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50 ये अहरोन के वंशज थे: उसका पुत्र एलिएज़र, उसका पुत्र फिनिहास, उसका पुत्र अबीशुआ,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51 उसका पुत्र बुक्की, उसका पुत्र उज्जी, ज़ेराइयाह.
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52 उसका पुत्र मेराइओथ, उसका पुत्र अमरियाह, उसका पुत्र अहीतूब,
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53 उसका पुत्र सादोक और उसका पुत्र अहीमाज़ था.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
54 उनकी सीमाओं ही के भीतर, उनके शिविरों के आधार पर उनके उपनिवेश इस प्रकार थे मतपत्रों के आधार पर सर्वप्रथम स्थान अहरोन के पुत्रों के परिवार को प्राप्त हुआ था. (अहरोन-वंशजों को जो कोहाथि कुल के थे, क्योंकि चिट्ठी डालकर वे ही इसके लिए पहले स्थान के लिए चुने गए थे):
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
55 इन्होंने उन्हें यहूदिया में हेब्रोन क्षेत्र दे दिया साथ ही इसके आस-पास के चरागाह भी.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
56 (किंतु नगर के बीच के खेत और इसके गांव उन्होंने येफुन्नेह के पुत्र कालेब को दे दिए.)
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 अहरोन के पुत्रों को उन्होंने शरण शहर दे दिए: हेब्रोन, लिबनाह और इसकी सभी चरागाह,
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
59 आशान, युताह और बेथ-शेमेश और उनकी चरागाह,
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
60 तब बिन्यामिन गोत्र की सीमा से गिबियोन, इसके चरागाहों से इसके चरागाहों समेत गेबा, अलेमेथ, अनाथोथ इसके सभी उनके ये सभी नगर उनके गोत्रों के अधिकार में हमेशा ही बने रहे. ये कुल तेरह नगर थे.
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
61 तब कोहाथ की शेष संतान को ये चिट्ठी डालकर बांट दिए गए. परिवार के गोत्र से, अर्धकुल से, मनश्शेह के आधे गोत्र से, दस नगर.
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
62 गेरशोम के पुत्रों को उनके परिवार के अनुसार इस्साखार के गोत्र में से, आशेर के गोत्र में से, नफताली के गोत्र में से और बाशान में मनश्शेह के गोत्र में से तेरह नगर प्रदान किए गए.
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 मेरारी वंशजों को उनके कुलों के अनुसार रियूबेन के, गाद के और ज़ेबुलून के कुलों से बारह नगर बांटे गए.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
64 इस प्रकार इस्राएल वंशजों को वे नगर दे दिए, जिनमें चरागाह भी थे.
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
65 यहूदाह गोत्र के कुलों से उन्होंने चिट्ठियों द्वारा शिमओन वंश के कुलों और बिन्यामिन वंश के कुलों को ये नगर, जिनका उल्लेख किया जा चुका है, दे दिए.
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
66 कोहाथ वंश के कुछ परिवारों के पास एफ्राईम गोत्र की सीमा में के कुछ नगर थे.
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
67 उन्होंने इन्हें ये शरण शहर दे दिए: एफ्राईम के पर्वतीय क्षेत्र का शेकेम और इसके चरागाहों के साथ गेज़ेर,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
69 चरागाहों के साथ अय्जालोन, चरागाहों के साथ गथ-रिम्मोन.
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
70 तब मनश्शेह के आधे गोत्र में से चरागाहों के साथ ऐनर और चरागाहों के साथ बिलआम.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
71 मनश्शेह के अर्ध-गोत्र में से गेरशोन-वंशजों को चरागाहों के साथ बाशान क्षेत्र में गोलान और चरागाहों के साथ अश्तारोथ;
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
72 इस्साखार के गोत्र में से चरागाहों के साथ के देश, चरागाहों के साथ दाबरथ,
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
73 चरागाहों के साथ रामोथ, चरागाहों के साथ आनेम;
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
74 आशेर के गोत्र से चरागाहों के साथ माशाल, चरागाहों के साथ अबदोन,
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
75 चरागाहों के साथ हूक्कोक और चरागाहों के साथ रेहोब;
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
76 नफताली के गोत्र में से चरागाहों के साथ गलील में केदेश, चरागाहों के साथ हम्मोन और चरागाहों के साथ किरयथियों.
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
77 मेरारी-वंशज शेष लेवियों को: ज़ेबुलून के गोत्र में से चरागाहों के साथ रिम्मोन, चरागाहों के साथ ताबोर;
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
78 और यरदन पार येरीख़ो में यरदन के पूर्वी तट पर रियूबेन के गोत्र में से चरागाहों के साथ बेज़र, जो बंजर भूमि में था, चरागाहों कि साथ यहत्स,
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
79 चरागाहों के साथ केदेमोथ और चरागाहों के साथ मेफाअथ;
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
80 गाद के गोत्र में से चरागाहों के साथ गिलआद में रामोथ, चरागाहों के साथ माहानाईम,
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
81 चरागाहों के साथ हेशबोन और याज़र.
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.