< אֶל־טִיטוֹס 3 >
הזכר אתם להכנע ולשמע לשרים ולשלטונים ולהיות נכונים לכל מעשה טוב׃ | 1 |
Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
ולבלתי גדף אדם ולחדל מריב ולהכריע לכף זכות ולהתנהג בכל ענוה לפני כל אדם׃ | 2 |
Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
כי גם אנחנו היינו מלפנים חסרי דעת וסוררים ותועים ועבדים לתאות ולתשוקות שנות ומתהלכים ברשעה וקנאה ושנואים ושנאים איש את אחיו׃ | 3 |
Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
אמנם כאשר נגלה נעם אלהים מושיענו ורחמנותו אל האדם׃ | 4 |
Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
אז לא בגלל מעשי הצדקה אשר עשינו הושיע אתנו כי אם מתוך חסדו על ידי טבילת התולדה השניה וחדוש רוח הקדש׃ | 5 |
alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
אשר שפך עלינו למכביר על ידי ישוע המשיח מושיענו׃ | 6 |
ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
למען נצדק בחסדו ונירש לפי התקוה את חיי העולמים׃ (aiōnios ) | 7 |
ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios )
נאמן הוא הדבר ורצה אני כי תקים את אלה למען אשר ישתדלו המאמינים לאלהים לעשק במעשים טובים עשות כאלה טוב הוא ומועיל לאדם׃ | 8 |
Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
אבל תרחק מן השאלות התפלות ומלמודי תולדות ומן הקטטות ומחלקות בעניני החקים כי אין בהן מועיל והבל הנה׃ | 9 |
Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
ואיש החולק על האמונה אם הוכח פעם ושתים שטה מעליו׃ | 10 |
Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
ודע כי איש כזה איש תהפכות הוא וחוטא בהרשיע את נפשו׃ | 11 |
Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
כאשר אשלח אליך את ארטמס או את טוכיקוס תמהר לבוא אלי לניקפליס כי גמרתי בלבי לשבת שם בימי הסתיו׃ | 12 |
Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
השתדל ללות על דרכם את זינס המלמד בתורה ואת אפולוס למען לא יחסרו דבר׃ | 13 |
Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
וילמדו גם אנשי עדתנו לעשק במעשים טובים לעזר בכל מחסור פן יהיו בלי פרי׃ | 14 |
Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
כל אשר עמדי שאלים לשלומך שאל לשלום האהבים אתנו באמונה החסד עם כלכם אמן׃ | 15 |
Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.