< תהילים 96 >
שירו ליהוה שיר חדש שירו ליהוה כל הארץ׃ | 1 |
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
שירו ליהוה ברכו שמו בשרו מיום ליום ישועתו׃ | 2 |
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
ספרו בגוים כבודו בכל העמים נפלאותיו׃ | 3 |
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
כי גדול יהוה ומהלל מאד נורא הוא על כל אלהים׃ | 4 |
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
כי כל אלהי העמים אלילים ויהוה שמים עשה׃ | 5 |
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
הוד והדר לפניו עז ותפארת במקדשו׃ | 6 |
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
הבו ליהוה משפחות עמים הבו ליהוה כבוד ועז׃ | 7 |
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
הבו ליהוה כבוד שמו שאו מנחה ובאו לחצרותיו׃ | 8 |
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
השתחוו ליהוה בהדרת קדש חילו מפניו כל הארץ׃ | 9 |
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
אמרו בגוים יהוה מלך אף תכון תבל בל תמוט ידין עמים במישרים׃ | 10 |
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
ישמחו השמים ותגל הארץ ירעם הים ומלאו׃ | 11 |
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
יעלז שדי וכל אשר בו אז ירננו כל עצי יער׃ | 12 |
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
לפני יהוה כי בא כי בא לשפט הארץ ישפט תבל בצדק ועמים באמונתו׃ | 13 |
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.