< תהילים 96 >

שירו ליהוה שיר חדש שירו ליהוה כל הארץ׃ 1
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
שירו ליהוה ברכו שמו בשרו מיום ליום ישועתו׃ 2
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
ספרו בגוים כבודו בכל העמים נפלאותיו׃ 3
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
כי גדול יהוה ומהלל מאד נורא הוא על כל אלהים׃ 4
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
כי כל אלהי העמים אלילים ויהוה שמים עשה׃ 5
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
הוד והדר לפניו עז ותפארת במקדשו׃ 6
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
הבו ליהוה משפחות עמים הבו ליהוה כבוד ועז׃ 7
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
הבו ליהוה כבוד שמו שאו מנחה ובאו לחצרותיו׃ 8
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
השתחוו ליהוה בהדרת קדש חילו מפניו כל הארץ׃ 9
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
אמרו בגוים יהוה מלך אף תכון תבל בל תמוט ידין עמים במישרים׃ 10
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
ישמחו השמים ותגל הארץ ירעם הים ומלאו׃ 11
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
יעלז שדי וכל אשר בו אז ירננו כל עצי יער׃ 12
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
לפני יהוה כי בא כי בא לשפט הארץ ישפט תבל בצדק ועמים באמונתו׃ 13
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< תהילים 96 >