< תהילים 92 >

מזמור שיר ליום השבת טוב להדות ליהוה ולזמר לשמך עליון׃ 1
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato. Ni vyema kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
להגיד בבקר חסדך ואמונתך בלילות׃ 2
kuutangaza upendo wako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku,
עלי עשור ועלי נבל עלי הגיון בכנור׃ 3
kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.
כי שמחתני יהוה בפעלך במעשי ידיך ארנן׃ 4
Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.
מה גדלו מעשיך יהוה מאד עמקו מחשבתיך׃ 5
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
איש בער לא ידע וכסיל לא יבין את זאת׃ 6
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
בפרח רשעים כמו עשב ויציצו כל פעלי און להשמדם עדי עד׃ 7
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
ואתה מרום לעלם יהוה׃ 8
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
כי הנה איביך יהוה כי הנה איביך יאבדו יתפרדו כל פעלי און׃ 9
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
ותרם כראים קרני בלתי בשמן רענן׃ 10
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
ותבט עיני בשורי בקמים עלי מרעים תשמענה אזני׃ 11
Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.
צדיק כתמר יפרח כארז בלבנון ישגה׃ 12
Wenye haki watastawi kama mtende, watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,
שתולים בבית יהוה בחצרות אלהינו יפריחו׃ 13
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
עוד ינובון בשיבה דשנים ורעננים יהיו׃ 14
Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,
להגיד כי ישר יהוה צורי ולא עלתה בו׃ 15
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”

< תהילים 92 >