< תהילים 92 >
מזמור שיר ליום השבת טוב להדות ליהוה ולזמר לשמך עליון׃ | 1 |
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato. Ni vyema kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
להגיד בבקר חסדך ואמונתך בלילות׃ | 2 |
kuutangaza upendo wako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku,
עלי עשור ועלי נבל עלי הגיון בכנור׃ | 3 |
kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.
כי שמחתני יהוה בפעלך במעשי ידיך ארנן׃ | 4 |
Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.
מה גדלו מעשיך יהוה מאד עמקו מחשבתיך׃ | 5 |
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
איש בער לא ידע וכסיל לא יבין את זאת׃ | 6 |
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
בפרח רשעים כמו עשב ויציצו כל פעלי און להשמדם עדי עד׃ | 7 |
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
כי הנה איביך יהוה כי הנה איביך יאבדו יתפרדו כל פעלי און׃ | 9 |
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
ותרם כראים קרני בלתי בשמן רענן׃ | 10 |
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
ותבט עיני בשורי בקמים עלי מרעים תשמענה אזני׃ | 11 |
Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.
צדיק כתמר יפרח כארז בלבנון ישגה׃ | 12 |
Wenye haki watastawi kama mtende, watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,
שתולים בבית יהוה בחצרות אלהינו יפריחו׃ | 13 |
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
עוד ינובון בשיבה דשנים ורעננים יהיו׃ | 14 |
Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,
להגיד כי ישר יהוה צורי ולא עלתה בו׃ | 15 |
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”