< תהילים 9 >
למנצח עלמות לבן מזמור לדוד אודה יהוה בכל לבי אספרה כל נפלאותיך׃ | 1 |
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa muth-labeni. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote, nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
אשמחה ואעלצה בך אזמרה שמך עליון׃ | 2 |
Nitafurahi na kushangilia ndani yako. Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.
בשוב אויבי אחור יכשלו ויאבדו מפניך׃ | 3 |
Adui zangu wamerudi nyuma, wamejikwaa na kuangamia mbele zako.
כי עשית משפטי ודיני ישבת לכסא שופט צדק׃ | 4 |
Kwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu; umeketi kwenye kiti chako cha enzi, ukihukumu kwa haki.
גערת גוים אבדת רשע שמם מחית לעולם ועד׃ | 5 |
Umekemea mataifa na kuwaangamiza waovu; umeyafuta majina yao milele na milele.
האויב תמו חרבות לנצח וערים נתשת אבד זכרם המה׃ | 6 |
Uharibifu usiokoma umempata adui, umeingʼoa miji yao; hata kumbukumbu lao limetoweka.
ויהוה לעולם ישב כונן למשפט כסאו׃ | 7 |
Bwana anatawala milele, ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.
והוא ישפט תבל בצדק ידין לאמים במישרים׃ | 8 |
Mungu atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kwa haki.
ויהי יהוה משגב לדך משגב לעתות בצרה׃ | 9 |
Bwana ni kimbilio la watu wanaoonewa, ni ngome imara wakati wa shida.
ויבטחו בך יודעי שמך כי לא עזבת דרשיך יהוה׃ | 10 |
Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe, kwa maana wewe Bwana, hujawaacha kamwe wakutafutao.
זמרו ליהוה ישב ציון הגידו בעמים עלילותיו׃ | 11 |
Mwimbieni Bwana sifa, amefanywa mtawala Sayuni, tangazeni miongoni mwa mataifa, yale aliyoyatenda.
כי דרש דמים אותם זכר לא שכח צעקת עניים׃ | 12 |
Kwa maana yeye alipizaye kisasi cha damu hukumbuka, hapuuzi kilio cha wanaoonewa.
חננני יהוה ראה עניי משנאי מרוממי משערי מות׃ | 13 |
Ee Bwana, tazama jinsi walivyo wengi adui zangu wanaonitesa! Nihurumie, uniinue kutoka malango ya mauti,
למען אספרה כל תהלתיך בשערי בת ציון אגילה בישועתך׃ | 14 |
ili niweze kutangaza sifa zako katika malango ya Binti Sayuni na huko niushangilie wokovu wako.
טבעו גוים בשחת עשו ברשת זו טמנו נלכדה רגלם׃ | 15 |
Mataifa wameanguka kwenye shimo walilolichimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliouficha.
נודע יהוה משפט עשה בפעל כפיו נוקש רשע הגיון סלה׃ | 16 |
Bwana anajulikana kwa haki yake, waovu wamenaswa katika kazi za mikono yao.
ישובו רשעים לשאולה כל גוים שכחי אלהים׃ (Sheol ) | 17 |
Waovu wataishia kuzimu, naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu. (Sheol )
כי לא לנצח ישכח אביון תקות ענוים תאבד לעד׃ | 18 |
Lakini mhitaji hatasahaulika siku zote, wala matumaini ya walioonewa hayatapotea.
קומה יהוה אל יעז אנוש ישפטו גוים על פניך׃ | 19 |
Ee Bwana, inuka, usimwache binadamu ashinde. Mataifa na yahukumiwe mbele zako.
שיתה יהוה מורה להם ידעו גוים אנוש המה סלה׃ | 20 |
Ee Bwana, wapige kwa hofu, mataifa na yajue kuwa wao ni watu tu.