< תהילים 86 >

תפלה לדוד הטה יהוה אזנך ענני כי עני ואביון אני׃ 1
Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
שמרה נפשי כי חסיד אני הושע עבדך אתה אלהי הבוטח אליך׃ 2
Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
חנני אדני כי אליך אקרא כל היום׃ 3
Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
שמח נפש עבדך כי אליך אדני נפשי אשא׃ 4
Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
כי אתה אדני טוב וסלח ורב חסד לכל קראיך׃ 5
Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
האזינה יהוה תפלתי והקשיבה בקול תחנונותי׃ 6
Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
ביום צרתי אקראך כי תענני׃ 7
Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
אין כמוך באלהים אדני ואין כמעשיך׃ 8
Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
כל גוים אשר עשית יבואו וישתחוו לפניך אדני ויכבדו לשמך׃ 9
Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
כי גדול אתה ועשה נפלאות אתה אלהים לבדך׃ 10
Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
הורני יהוה דרכך אהלך באמתך יחד לבבי ליראה שמך׃ 11
Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
אודך אדני אלהי בכל לבבי ואכבדה שמך לעולם׃ 12
Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
כי חסדך גדול עלי והצלת נפשי משאול תחתיה׃ (Sheol h7585) 13
Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol h7585)
אלהים זדים קמו עלי ועדת עריצים בקשו נפשי ולא שמוך לנגדם׃ 14
Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
ואתה אדני אל רחום וחנון ארך אפים ורב חסד ואמת׃ 15
Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
פנה אלי וחנני תנה עזך לעבדך והושיעה לבן אמתך׃ 16
Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
עשה עמי אות לטובה ויראו שנאי ויבשו כי אתה יהוה עזרתני ונחמתני׃ 17
Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.

< תהילים 86 >