< תהילים 86 >
תפלה לדוד הטה יהוה אזנך ענני כי עני ואביון אני׃ | 1 |
Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
שמרה נפשי כי חסיד אני הושע עבדך אתה אלהי הבוטח אליך׃ | 2 |
Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
חנני אדני כי אליך אקרא כל היום׃ | 3 |
Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
שמח נפש עבדך כי אליך אדני נפשי אשא׃ | 4 |
Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
כי אתה אדני טוב וסלח ורב חסד לכל קראיך׃ | 5 |
Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
האזינה יהוה תפלתי והקשיבה בקול תחנונותי׃ | 6 |
Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
ביום צרתי אקראך כי תענני׃ | 7 |
Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
אין כמוך באלהים אדני ואין כמעשיך׃ | 8 |
Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
כל גוים אשר עשית יבואו וישתחוו לפניך אדני ויכבדו לשמך׃ | 9 |
Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
כי גדול אתה ועשה נפלאות אתה אלהים לבדך׃ | 10 |
Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
הורני יהוה דרכך אהלך באמתך יחד לבבי ליראה שמך׃ | 11 |
Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
אודך אדני אלהי בכל לבבי ואכבדה שמך לעולם׃ | 12 |
Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
כי חסדך גדול עלי והצלת נפשי משאול תחתיה׃ (Sheol ) | 13 |
Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol )
אלהים זדים קמו עלי ועדת עריצים בקשו נפשי ולא שמוך לנגדם׃ | 14 |
Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
ואתה אדני אל רחום וחנון ארך אפים ורב חסד ואמת׃ | 15 |
Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
פנה אלי וחנני תנה עזך לעבדך והושיעה לבן אמתך׃ | 16 |
Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
עשה עמי אות לטובה ויראו שנאי ויבשו כי אתה יהוה עזרתני ונחמתני׃ | 17 |
Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.