< תהילים 83 >
שיר מזמור לאסף אלהים אל דמי לך אל תחרש ואל תשקט אל׃ | 1 |
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
כי הנה אויביך יהמיון ומשנאיך נשאו ראש׃ | 2 |
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
על עמך יערימו סוד ויתיעצו על צפוניך׃ | 3 |
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
אמרו לכו ונכחידם מגוי ולא יזכר שם ישראל עוד׃ | 4 |
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
כי נועצו לב יחדו עליך ברית יכרתו׃ | 5 |
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
אהלי אדום וישמעאלים מואב והגרים׃ | 6 |
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
גבל ועמון ועמלק פלשת עם ישבי צור׃ | 7 |
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
גם אשור נלוה עמם היו זרוע לבני לוט סלה׃ | 8 |
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
עשה להם כמדין כסיסרא כיבין בנחל קישון׃ | 9 |
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
נשמדו בעין דאר היו דמן לאדמה׃ | 10 |
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
שיתמו נדיבמו כערב וכזאב וכזבח וכצלמנע כל נסיכמו׃ | 11 |
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
אשר אמרו נירשה לנו את נאות אלהים׃ | 12 |
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
אלהי שיתמו כגלגל כקש לפני רוח׃ | 13 |
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
כאש תבער יער וכלהבה תלהט הרים׃ | 14 |
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
כן תרדפם בסערך ובסופתך תבהלם׃ | 15 |
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
מלא פניהם קלון ויבקשו שמך יהוה׃ | 16 |
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
יבשו ויבהלו עדי עד ויחפרו ויאבדו׃ | 17 |
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
וידעו כי אתה שמך יהוה לבדך עליון על כל הארץ׃ | 18 |
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.