< תהילים 75 >
למנצח אל תשחת מזמור לאסף שיר הודינו לך אלהים הודינו וקרוב שמך ספרו נפלאותיך׃ | 1 |
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
כי אקח מועד אני מישרים אשפט׃ | 2 |
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
נמגים ארץ וכל ישביה אנכי תכנתי עמודיה סלה׃ | 3 |
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
אמרתי להוללים אל תהלו ולרשעים אל תרימו קרן׃ | 4 |
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
אל תרימו למרום קרנכם תדברו בצואר עתק׃ | 5 |
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
כי לא ממוצא וממערב ולא ממדבר הרים׃ | 6 |
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
כי אלהים שפט זה ישפיל וזה ירים׃ | 7 |
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
כי כוס ביד יהוה ויין חמר מלא מסך ויגר מזה אך שמריה ימצו ישתו כל רשעי ארץ׃ | 8 |
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
ואני אגיד לעלם אזמרה לאלהי יעקב׃ | 9 |
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
וכל קרני רשעים אגדע תרוממנה קרנות צדיק׃ | 10 |
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.