< תהילים 7 >
שגיון לדוד אשר שר ליהוה על דברי כוש בן ימיני יהוה אלהי בך חסיתי הושיעני מכל רדפי והצילני׃ | 1 |
Yahweh Mungu wangu, kwako napata kimbilio! Uninusuru na hao wote wanikimbizao, na uniokoe.
פן יטרף כאריה נפשי פרק ואין מציל׃ | 2 |
Vinginevyo, watanipura kama simba, na kunitawanya viapande vipande na asiwepo mtu wa kuweza kunirudisha katika usalama.
יהוה אלהי אם עשיתי זאת אם יש עול בכפי׃ | 3 |
Yawheh Mungu wangu, Sijawahi kufanya kile maadui zangu wanacho sema nilifanya; sina hatia katika mikono yangu.
אם גמלתי שולמי רע ואחלצה צוררי ריקם׃ | 4 |
Sijawahi kumkosea mtu yeyote aliye na amani na mimi, au kumdhuru kipumbavu yeyote aliye kinyume na mimi.
ירדף אויב נפשי וישג וירמס לארץ חיי וכבודי לעפר ישכן סלה׃ | 5 |
Ikiwa sisemi ukweli basi umruhusu adui yangu kuyaingilia maisha yangu na kuyaharibu; na umuache aukanyage mwili wangu ulio hai kwenye aridhi na kuuacha umelala kwa aibu mavumbini. (Selah)
קומה יהוה באפך הנשא בעברות צוררי ועורה אלי משפט צוית׃ | 6 |
Inuka, Yahweh, katika hasira yako; simama kinyume na hasira kali ya adui zangu; amka kwa ajili yangu na ubebe amri zako ambazo wewe umeamuru kwa ajili yao.
ועדת לאמים תסובבך ועליה למרום שובה׃ | 7 |
Mataifa yote yamekuzunguka; uwatawale kutoka mbinguni.
יהוה ידין עמים שפטני יהוה כצדקי וכתמי עלי׃ | 8 |
Yahweh, uwahukumu mataifa; uwaonyeshe kuwa sina hatia, Yahweh, kwa sababu mimi ni mwenye haki na sina hatia, Ewe uliye juu.
יגמר נא רע רשעים ותכונן צדיק ובחן לבות וכליות אלהים צדיק׃ | 9 |
Matendo ya waovu na yafike mwisho, bali uanzishe watu wenye haki, Mungu mwenye haki, wewe ambaye unapima mioyo na fahamu.
מגני על אלהים מושיע ישרי לב׃ | 10 |
Ngao yangu inatoka kwa Mungu, yule anaye okoa moyo wa mwenye haki.
אלהים שופט צדיק ואל זעם בכל יום׃ | 11 |
Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu anaye chukizwa na waovu kila siku.
אם לא ישוב חרבו ילטוש קשתו דרך ויכוננה׃ | 12 |
Ikiwa kuna mtu hatubu, Mungu atanoa upanga wake na ata andaa upinde wake kwa ajili ya vita.
ולו הכין כלי מות חציו לדלקים יפעל׃ | 13 |
Ana jiandaa kutumia siraha kupambana naye; anatengeneza mishale yake kuwa ya moto.
הנה יחבל און והרה עמל וילד שקר׃ | 14 |
Fikiria kuhusu huyo ambaye ana ujauzito wa maovu, mwenye mimba ya mipango ya uharibifu, anaye zaa sumu ya uharibifu.
בור כרה ויחפרהו ויפל בשחת יפעל׃ | 15 |
Yeye huchimba shimo na kuliacha wazi kisha baadaye hudumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
ישוב עמלו בראשו ועל קדקדו חמסו ירד׃ | 16 |
Mipango yake mwenyewe ya uharibifu hugeukia kichwa chake mwenyewe, kwa kuwa vurugu zake mwenyewe humshukia kichwani pake.
אודה יהוה כצדקו ואזמרה שם יהוה עליון׃ | 17 |
Kwa haki yako Mungu nitakushukuru; nitaimba sifa kwa Mungu aliye juu.