< תהילים 7 >

שגיון לדוד אשר שר ליהוה על דברי כוש בן ימיני יהוה אלהי בך חסיתי הושיעני מכל רדפי והצילני׃ 1
Yahweh Mungu wangu, kwako napata kimbilio! Uninusuru na hao wote wanikimbizao, na uniokoe.
פן יטרף כאריה נפשי פרק ואין מציל׃ 2
Vinginevyo, watanipura kama simba, na kunitawanya viapande vipande na asiwepo mtu wa kuweza kunirudisha katika usalama.
יהוה אלהי אם עשיתי זאת אם יש עול בכפי׃ 3
Yawheh Mungu wangu, Sijawahi kufanya kile maadui zangu wanacho sema nilifanya; sina hatia katika mikono yangu.
אם גמלתי שולמי רע ואחלצה צוררי ריקם׃ 4
Sijawahi kumkosea mtu yeyote aliye na amani na mimi, au kumdhuru kipumbavu yeyote aliye kinyume na mimi.
ירדף אויב נפשי וישג וירמס לארץ חיי וכבודי לעפר ישכן סלה׃ 5
Ikiwa sisemi ukweli basi umruhusu adui yangu kuyaingilia maisha yangu na kuyaharibu; na umuache aukanyage mwili wangu ulio hai kwenye aridhi na kuuacha umelala kwa aibu mavumbini. (Selah)
קומה יהוה באפך הנשא בעברות צוררי ועורה אלי משפט צוית׃ 6
Inuka, Yahweh, katika hasira yako; simama kinyume na hasira kali ya adui zangu; amka kwa ajili yangu na ubebe amri zako ambazo wewe umeamuru kwa ajili yao.
ועדת לאמים תסובבך ועליה למרום שובה׃ 7
Mataifa yote yamekuzunguka; uwatawale kutoka mbinguni.
יהוה ידין עמים שפטני יהוה כצדקי וכתמי עלי׃ 8
Yahweh, uwahukumu mataifa; uwaonyeshe kuwa sina hatia, Yahweh, kwa sababu mimi ni mwenye haki na sina hatia, Ewe uliye juu.
יגמר נא רע רשעים ותכונן צדיק ובחן לבות וכליות אלהים צדיק׃ 9
Matendo ya waovu na yafike mwisho, bali uanzishe watu wenye haki, Mungu mwenye haki, wewe ambaye unapima mioyo na fahamu.
מגני על אלהים מושיע ישרי לב׃ 10
Ngao yangu inatoka kwa Mungu, yule anaye okoa moyo wa mwenye haki.
אלהים שופט צדיק ואל זעם בכל יום׃ 11
Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu anaye chukizwa na waovu kila siku.
אם לא ישוב חרבו ילטוש קשתו דרך ויכוננה׃ 12
Ikiwa kuna mtu hatubu, Mungu atanoa upanga wake na ata andaa upinde wake kwa ajili ya vita.
ולו הכין כלי מות חציו לדלקים יפעל׃ 13
Ana jiandaa kutumia siraha kupambana naye; anatengeneza mishale yake kuwa ya moto.
הנה יחבל און והרה עמל וילד שקר׃ 14
Fikiria kuhusu huyo ambaye ana ujauzito wa maovu, mwenye mimba ya mipango ya uharibifu, anaye zaa sumu ya uharibifu.
בור כרה ויחפרהו ויפל בשחת יפעל׃ 15
Yeye huchimba shimo na kuliacha wazi kisha baadaye hudumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
ישוב עמלו בראשו ועל קדקדו חמסו ירד׃ 16
Mipango yake mwenyewe ya uharibifu hugeukia kichwa chake mwenyewe, kwa kuwa vurugu zake mwenyewe humshukia kichwani pake.
אודה יהוה כצדקו ואזמרה שם יהוה עליון׃ 17
Kwa haki yako Mungu nitakushukuru; nitaimba sifa kwa Mungu aliye juu.

< תהילים 7 >