< תהילים 69 >
למנצח על שושנים לדוד הושיעני אלהים כי באו מים עד נפש׃ | 1 |
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni.
טבעתי ביון מצולה ואין מעמד באתי במעמקי מים ושבלת שטפתני׃ | 2 |
Ninazama kwenye vilindi vya matope, pasipo mahali pa kukanyaga, Nimefika kwenye maji makuu, mafuriko yamenigharikisha.
יגעתי בקראי נחר גרוני כלו עיני מיחל לאלהי׃ | 3 |
Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.
רבו משערות ראשי שנאי חנם עצמו מצמיתי איבי שקר אשר לא גזלתי אז אשיב׃ | 4 |
Wale wanaonichukia bila sababu ni wengi kuliko nywele za kichwa changu; wengi ni adui kwangu bila sababu, wale wanaotafuta kuniangamiza. Ninalazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.
אלהים אתה ידעת לאולתי ואשמותי ממך לא נכחדו׃ | 5 |
Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu, wala hatia yangu haikufichika kwako.
אל יבשו בי קויך אדני יהוה צבאות אל יכלמו בי מבקשיך אלהי ישראל׃ | 6 |
Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote, wakutumainio wasiaibishwe kwa ajili yangu; wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.
כי עליך נשאתי חרפה כסתה כלמה פני׃ | 7 |
Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako, aibu imefunika uso wangu.
מוזר הייתי לאחי ונכרי לבני אמי׃ | 8 |
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
כי קנאת ביתך אכלתני וחרפות חורפיך נפלו עלי׃ | 9 |
Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila, matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
ואבכה בצום נפשי ותהי לחרפות לי׃ | 10 |
Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.
ואתנה לבושי שק ואהי להם למשל׃ | 11 |
Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.
ישיחו בי ישבי שער ונגינות שותי שכר׃ | 12 |
Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.
ואני תפלתי לך יהוה עת רצון אלהים ברב חסדך ענני באמת ישעך׃ | 13 |
Lakini Ee Bwana, ninakuomba, kwa wakati ukupendezao; katika upendo wako mkuu, Ee Mungu, unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
הצילני מטיט ואל אטבעה אנצלה משנאי וממעמקי מים׃ | 14 |
Uniokoe katika matope, usiniache nizame; niokoe na hao wanichukiao, kutoka kwenye vilindi vya maji.
אל תשטפני שבלת מים ואל תבלעני מצולה ואל תאטר עלי באר פיה׃ | 15 |
Usiache mafuriko yanigharikishe au vilindi vinimeze, au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
ענני יהוה כי טוב חסדך כרב רחמיך פנה אלי׃ | 16 |
Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako; kwa huruma zako nyingi unigeukie.
ואל תסתר פניך מעבדך כי צר לי מהר ענני׃ | 17 |
Usimfiche mtumishi wako uso wako, uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
קרבה אל נפשי גאלה למען איבי פדני׃ | 18 |
Njoo karibu uniokoe, nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
אתה ידעת חרפתי ובשתי וכלמתי נגדך כל צוררי׃ | 19 |
Unajua jinsi ninavyodharauliwa, kufedheheshwa na kuaibishwa, adui zangu wote unawajua.
חרפה שברה לבי ואנושה ואקוה לנוד ואין ולמנחמים ולא מצאתי׃ | 20 |
Dharau zimenivunja moyo na nimekata tamaa, nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata, wa kunituliza, lakini sikumpata.
ויתנו בברותי ראש ולצמאי ישקוני חמץ׃ | 21 |
Waliweka nyongo katika chakula changu na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
יהי שלחנם לפניהם לפח ולשלומים למוקש׃ | 22 |
Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego, nayo iwe upatilizo na tanzi.
תחשכנה עיניהם מראות ומתניהם תמיד המעד׃ | 23 |
Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.
שפך עליהם זעמך וחרון אפך ישיגם׃ | 24 |
Uwamwagie ghadhabu yako, hasira yako kali na iwapate.
תהי טירתם נשמה באהליהם אל יהי ישב׃ | 25 |
Mahali pao na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
כי אתה אשר הכית רדפו ואל מכאוב חלליך יספרו׃ | 26 |
Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi, na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
תנה עון על עונם ואל יבאו בצדקתך׃ | 27 |
Walipize uovu juu ya uovu, usiwaache washiriki katika wokovu wako.
ימחו מספר חיים ועם צדיקים אל יכתבו׃ | 28 |
Wafutwe kutoka kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
ואני עני וכואב ישועתך אלהים תשגבני׃ | 29 |
Mimi niko katika maumivu na dhiki; Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
אהללה שם אלהים בשיר ואגדלנו בתודה׃ | 30 |
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
ותיטב ליהוה משור פר מקרן מפריס׃ | 31 |
Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume, zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
ראו ענוים ישמחו דרשי אלהים ויחי לבבכם׃ | 32 |
Maskini wataona na kufurahi: ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
כי שמע אל אביונים יהוה ואת אסיריו לא בזה׃ | 33 |
Bwana huwasikia wahitaji wala hadharau watu wake waliotekwa.
יהללוהו שמים וארץ ימים וכל רמש בם׃ | 34 |
Mbingu na dunia zimsifu, bahari na vyote viendavyo ndani yake,
כי אלהים יושיע ציון ויבנה ערי יהודה וישבו שם וירשוה׃ | 35 |
kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na kuijenga tena miji ya Yuda. Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
וזרע עבדיו ינחלוה ואהבי שמו ישכנו בה׃ | 36 |
watoto wa watumishi wake watairithi na wale wote walipendao jina lake wataishi humo.