< תהילים 69 >

למנצח על שושנים לדוד הושיעני אלהים כי באו מים עד נפש׃ 1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni.
טבעתי ביון מצולה ואין מעמד באתי במעמקי מים ושבלת שטפתני׃ 2
Ninazama kwenye vilindi vya matope, pasipo mahali pa kukanyaga, Nimefika kwenye maji makuu, mafuriko yamenigharikisha.
יגעתי בקראי נחר גרוני כלו עיני מיחל לאלהי׃ 3
Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.
רבו משערות ראשי שנאי חנם עצמו מצמיתי איבי שקר אשר לא גזלתי אז אשיב׃ 4
Wale wanaonichukia bila sababu ni wengi kuliko nywele za kichwa changu; wengi ni adui kwangu bila sababu, wale wanaotafuta kuniangamiza. Ninalazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.
אלהים אתה ידעת לאולתי ואשמותי ממך לא נכחדו׃ 5
Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu, wala hatia yangu haikufichika kwako.
אל יבשו בי קויך אדני יהוה צבאות אל יכלמו בי מבקשיך אלהי ישראל׃ 6
Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote, wakutumainio wasiaibishwe kwa ajili yangu; wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.
כי עליך נשאתי חרפה כסתה כלמה פני׃ 7
Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako, aibu imefunika uso wangu.
מוזר הייתי לאחי ונכרי לבני אמי׃ 8
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
כי קנאת ביתך אכלתני וחרפות חורפיך נפלו עלי׃ 9
Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila, matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
ואבכה בצום נפשי ותהי לחרפות לי׃ 10
Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.
ואתנה לבושי שק ואהי להם למשל׃ 11
Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.
ישיחו בי ישבי שער ונגינות שותי שכר׃ 12
Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.
ואני תפלתי לך יהוה עת רצון אלהים ברב חסדך ענני באמת ישעך׃ 13
Lakini Ee Bwana, ninakuomba, kwa wakati ukupendezao; katika upendo wako mkuu, Ee Mungu, unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
הצילני מטיט ואל אטבעה אנצלה משנאי וממעמקי מים׃ 14
Uniokoe katika matope, usiniache nizame; niokoe na hao wanichukiao, kutoka kwenye vilindi vya maji.
אל תשטפני שבלת מים ואל תבלעני מצולה ואל תאטר עלי באר פיה׃ 15
Usiache mafuriko yanigharikishe au vilindi vinimeze, au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
ענני יהוה כי טוב חסדך כרב רחמיך פנה אלי׃ 16
Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako; kwa huruma zako nyingi unigeukie.
ואל תסתר פניך מעבדך כי צר לי מהר ענני׃ 17
Usimfiche mtumishi wako uso wako, uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
קרבה אל נפשי גאלה למען איבי פדני׃ 18
Njoo karibu uniokoe, nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
אתה ידעת חרפתי ובשתי וכלמתי נגדך כל צוררי׃ 19
Unajua jinsi ninavyodharauliwa, kufedheheshwa na kuaibishwa, adui zangu wote unawajua.
חרפה שברה לבי ואנושה ואקוה לנוד ואין ולמנחמים ולא מצאתי׃ 20
Dharau zimenivunja moyo na nimekata tamaa, nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata, wa kunituliza, lakini sikumpata.
ויתנו בברותי ראש ולצמאי ישקוני חמץ׃ 21
Waliweka nyongo katika chakula changu na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
יהי שלחנם לפניהם לפח ולשלומים למוקש׃ 22
Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego, nayo iwe upatilizo na tanzi.
תחשכנה עיניהם מראות ומתניהם תמיד המעד׃ 23
Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.
שפך עליהם זעמך וחרון אפך ישיגם׃ 24
Uwamwagie ghadhabu yako, hasira yako kali na iwapate.
תהי טירתם נשמה באהליהם אל יהי ישב׃ 25
Mahali pao na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
כי אתה אשר הכית רדפו ואל מכאוב חלליך יספרו׃ 26
Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi, na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
תנה עון על עונם ואל יבאו בצדקתך׃ 27
Walipize uovu juu ya uovu, usiwaache washiriki katika wokovu wako.
ימחו מספר חיים ועם צדיקים אל יכתבו׃ 28
Wafutwe kutoka kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
ואני עני וכואב ישועתך אלהים תשגבני׃ 29
Mimi niko katika maumivu na dhiki; Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
אהללה שם אלהים בשיר ואגדלנו בתודה׃ 30
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
ותיטב ליהוה משור פר מקרן מפריס׃ 31
Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume, zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
ראו ענוים ישמחו דרשי אלהים ויחי לבבכם׃ 32
Maskini wataona na kufurahi: ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
כי שמע אל אביונים יהוה ואת אסיריו לא בזה׃ 33
Bwana huwasikia wahitaji wala hadharau watu wake waliotekwa.
יהללוהו שמים וארץ ימים וכל רמש בם׃ 34
Mbingu na dunia zimsifu, bahari na vyote viendavyo ndani yake,
כי אלהים יושיע ציון ויבנה ערי יהודה וישבו שם וירשוה׃ 35
kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na kuijenga tena miji ya Yuda. Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
וזרע עבדיו ינחלוה ואהבי שמו ישכנו בה׃ 36
watoto wa watumishi wake watairithi na wale wote walipendao jina lake wataishi humo.

< תהילים 69 >