< תהילים 64 >

למנצח מזמור לדוד שמע אלהים קולי בשיחי מפחד אויב תצר חיי׃ 1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
תסתירני מסוד מרעים מרגשת פעלי און׃ 2
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
אשר שננו כחרב לשונם דרכו חצם דבר מר׃ 3
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
לירות במסתרים תם פתאם ירהו ולא ייראו׃ 4
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
יחזקו למו דבר רע יספרו לטמון מוקשים אמרו מי יראה למו׃ 5
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
יחפשו עולת תמנו חפש מחפש וקרב איש ולב עמק׃ 6
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
וירם אלהים חץ פתאום היו מכותם׃ 7
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
ויכשילוהו עלימו לשונם יתנדדו כל ראה בם׃ 8
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
וייראו כל אדם ויגידו פעל אלהים ומעשהו השכילו׃ 9
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
ישמח צדיק ביהוה וחסה בו ויתהללו כל ישרי לב׃ 10
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

< תהילים 64 >