< תהילים 64 >
למנצח מזמור לדוד שמע אלהים קולי בשיחי מפחד אויב תצר חיי׃ | 1 |
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
תסתירני מסוד מרעים מרגשת פעלי און׃ | 2 |
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
אשר שננו כחרב לשונם דרכו חצם דבר מר׃ | 3 |
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
לירות במסתרים תם פתאם ירהו ולא ייראו׃ | 4 |
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
יחזקו למו דבר רע יספרו לטמון מוקשים אמרו מי יראה למו׃ | 5 |
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
יחפשו עולת תמנו חפש מחפש וקרב איש ולב עמק׃ | 6 |
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
וירם אלהים חץ פתאום היו מכותם׃ | 7 |
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
ויכשילוהו עלימו לשונם יתנדדו כל ראה בם׃ | 8 |
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
וייראו כל אדם ויגידו פעל אלהים ומעשהו השכילו׃ | 9 |
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
ישמח צדיק ביהוה וחסה בו ויתהללו כל ישרי לב׃ | 10 |
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!