< תהילים 5 >
למנצח אל הנחילות מזמור לדוד אמרי האזינה יהוה בינה הגיגי׃ | 1 |
Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
הקשיבה לקול שועי מלכי ואלהי כי אליך אתפלל׃ | 2 |
Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
יהוה בקר תשמע קולי בקר אערך לך ואצפה׃ | 3 |
Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
כי לא אל חפץ רשע אתה לא יגרך רע׃ | 4 |
Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
לא יתיצבו הוללים לנגד עיניך שנאת כל פעלי און׃ | 5 |
Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
תאבד דברי כזב איש דמים ומרמה יתעב יהוה׃ | 6 |
Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
ואני ברב חסדך אבוא ביתך אשתחוה אל היכל קדשך ביראתך׃ | 7 |
Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
יהוה נחני בצדקתך למען שוררי הושר לפני דרכך׃ | 8 |
Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
כי אין בפיהו נכונה קרבם הוות קבר פתוח גרונם לשונם יחליקון׃ | 9 |
Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
האשימם אלהים יפלו ממעצותיהם ברב פשעיהם הדיחמו כי מרו בך׃ | 10 |
Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
וישמחו כל חוסי בך לעולם ירננו ותסך עלימו ויעלצו בך אהבי שמך׃ | 11 |
Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
כי אתה תברך צדיק יהוה כצנה רצון תעטרנו׃ | 12 |
Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.