< תהילים 5 >

למנצח אל הנחילות מזמור לדוד אמרי האזינה יהוה בינה הגיגי׃ 1
Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
הקשיבה לקול שועי מלכי ואלהי כי אליך אתפלל׃ 2
Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
יהוה בקר תשמע קולי בקר אערך לך ואצפה׃ 3
Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
כי לא אל חפץ רשע אתה לא יגרך רע׃ 4
Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
לא יתיצבו הוללים לנגד עיניך שנאת כל פעלי און׃ 5
Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
תאבד דברי כזב איש דמים ומרמה יתעב יהוה׃ 6
Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
ואני ברב חסדך אבוא ביתך אשתחוה אל היכל קדשך ביראתך׃ 7
Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
יהוה נחני בצדקתך למען שוררי הושר לפני דרכך׃ 8
Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
כי אין בפיהו נכונה קרבם הוות קבר פתוח גרונם לשונם יחליקון׃ 9
Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
האשימם אלהים יפלו ממעצותיהם ברב פשעיהם הדיחמו כי מרו בך׃ 10
Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
וישמחו כל חוסי בך לעולם ירננו ותסך עלימו ויעלצו בך אהבי שמך׃ 11
Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
כי אתה תברך צדיק יהוה כצנה רצון תעטרנו׃ 12
Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.

< תהילים 5 >