< תהילים 39 >
למנצח לידיתון מזמור לדוד אמרתי אשמרה דרכי מחטוא בלשוני אשמרה לפי מחסום בעד רשע לנגדי׃ | 1 |
Niliamua, “Nitakuwa mwangalifu kwa kile nisemacho ili kwamba nisitende dhambi kwa ulimi wangu. Nitaufumba mdomo wangu niwapo uweponi mwa mtu mwovu.”
נאלמתי דומיה החשיתי מטוב וכאבי נעכר׃ | 2 |
Nilikaa kimya; Nilizuia maneno yangu hata kuongea lolote zuri, na maumivu yangu yalizidi sana.
חם לבי בקרבי בהגיגי תבער אש דברתי בלשוני׃ | 3 |
Moyo wangu ukawaka moto; nilipoyatafakari mambo haya, yaliniunguza kama moto. Ndipo mwishowe niliongea.
הודיעני יהוה קצי ומדת ימי מה היא אדעה מה חדל אני׃ | 4 |
Yahwe, unijulishe ni lini utakuwa mwisho wa maisha yangu na kiwango cha siku zangu. Unioneshe jinsi maisha yangu yalivyo mafupi.
הנה טפחות נתתה ימי וחלדי כאין נגדך אך כל הבל כל אדם נצב סלה׃ | 5 |
Tazama, wewe umezifanya siku zangu kama upana wa kiganja changu tu, sikuzangu za kuishi ni kama si kitu mbele zako. Hakika kila mtu ana pumzi moja. (Selah)
אך בצלם יתהלך איש אך הבל יהמיון יצבר ולא ידע מי אספם׃ | 6 |
Hakika kila mtu hutembea kama kivuli. Hakika kila mmoja hufanya haraka kuhusu kukusaya utajiri ingawa hawajui ni nani atazipokea.
ועתה מה קויתי אדני תוחלתי לך היא׃ | 7 |
Sasa, Bwana, ninasubiri kwa ajili ya nini? Wewe ni tumaini langu pekee.
מכל פשעי הצילני חרפת נבל אל תשימני׃ | 8 |
Uniokoe na dhambi zangu; usinifanye laumu ya wabumbavu.
נאלמתי לא אפתח פי כי אתה עשית׃ | 9 |
Niko kimya na siwezi kufungua mdomo wangu, kwa sababu ni wewe ndiwe umefanya hivyo.
הסר מעלי נגעך מתגרת ידך אני כליתי׃ | 10 |
Acha kunijeruhi; nimezidiwa na pigo la mkono wako.
בתוכחות על עון יסרת איש ותמס כעש חמודו אך הבל כל אדם סלה׃ | 11 |
Wewe unapowaadhibu watu kwa ajili ya dhambi, huvila kama nondo vitu vyao wavitamanivyo; hakika watu si kitu bali mvuke. Serah
שמעה תפלתי יהוה ושועתי האזינה אל דמעתי אל תחרש כי גר אנכי עמך תושב ככל אבותי׃ | 12 |
Sikia maombi yangu, Yahwe, na unisikilize; usikie kilio changu! Usiwe kiziwi kwangu, kwa maana niko kama mgeni pamoja nawe, kimbilio langu la usalama kama mababu zangu walivyokuwa.
השע ממני ואבליגה בטרם אלך ואינני׃ | 13 |
Geuzia furaha yako kwangu ili kwamba niweze kutabasamu kabla sijafa.