< תהילים 33 >
רננו צדיקים ביהוה לישרים נאוה תהלה׃ | 1 |
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
הודו ליהוה בכנור בנבל עשור זמרו לו׃ | 2 |
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
שירו לו שיר חדש היטיבו נגן בתרועה׃ | 3 |
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
כי ישר דבר יהוה וכל מעשהו באמונה׃ | 4 |
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
אהב צדקה ומשפט חסד יהוה מלאה הארץ׃ | 5 |
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
בדבר יהוה שמים נעשו וברוח פיו כל צבאם׃ | 6 |
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
כנס כנד מי הים נתן באצרות תהומות׃ | 7 |
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
ייראו מיהוה כל הארץ ממנו יגורו כל ישבי תבל׃ | 8 |
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
כי הוא אמר ויהי הוא צוה ויעמד׃ | 9 |
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
יהוה הפיר עצת גוים הניא מחשבות עמים׃ | 10 |
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
עצת יהוה לעולם תעמד מחשבות לבו לדר ודר׃ | 11 |
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
אשרי הגוי אשר יהוה אלהיו העם בחר לנחלה לו׃ | 12 |
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
משמים הביט יהוה ראה את כל בני האדם׃ | 13 |
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
ממכון שבתו השגיח אל כל ישבי הארץ׃ | 14 |
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
היצר יחד לבם המבין אל כל מעשיהם׃ | 15 |
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
אין המלך נושע ברב חיל גבור לא ינצל ברב כח׃ | 16 |
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
שקר הסוס לתשועה וברב חילו לא ימלט׃ | 17 |
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
הנה עין יהוה אל יראיו למיחלים לחסדו׃ | 18 |
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
להציל ממות נפשם ולחיותם ברעב׃ | 19 |
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
נפשנו חכתה ליהוה עזרנו ומגננו הוא׃ | 20 |
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
כי בו ישמח לבנו כי בשם קדשו בטחנו׃ | 21 |
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
יהי חסדך יהוה עלינו כאשר יחלנו לך׃ | 22 |
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.