< תהילים 30 >
מזמור שיר חנכת הבית לדוד ארוממך יהוה כי דליתני ולא שמחת איבי לי׃ | 1 |
Nitakutukuza wewe, Yahwe, kwa kuwa umeniinua na haujawaruhusu maadui zangu juu yangu.
יהוה אלהי שועתי אליך ותרפאני׃ | 2 |
Yahwe Mungu wangu, nilikulilia wewe kwa ajili ya msaada, nawe ukaniponya.
יהוה העלית מן שאול נפשי חייתני מיורדי בור׃ (Sheol ) | 3 |
Yahwe, wewe umeitoa roho yangu kuzimuni; nawe umeniweka hai mbali na kaburi. (Sheol )
זמרו ליהוה חסידיו והודו לזכר קדשו׃ | 4 |
Mwimbieni sifa Yahwe, ninyi waaminifu wake! Mshukuruni Bwana mkumbukapo utakatifu wake.
כי רגע באפו חיים ברצונו בערב ילין בכי ולבקר רנה׃ | 5 |
Kwa kuwa hasira yake ni ya muda tu; bali neema yake yadumu milele. Kilio huja usiku, bali furaha huja asubuhi.
ואני אמרתי בשלוי בל אמוט לעולם׃ | 6 |
Kwa ujasiri nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
יהוה ברצונך העמדתה להררי עז הסתרת פניך הייתי נבהל׃ | 7 |
Yahwe, kwa neema yako uliniweka mimi kama mlima imara; lakini ulipouficha uso wako, nilisumbuka.
אליך יהוה אקרא ואל אדני אתחנן׃ | 8 |
Nilikulilia wewe, Yahwe, na kuomba msaada kwa Bwana wangu!
מה בצע בדמי ברדתי אל שחת היודך עפר היגיד אמתך׃ | 9 |
Kuna faida gani katika kifo changu, kama nitaenda kaburini? Je, mavumbi yatakusifu wewe? Yatatangaza uaminifu wako?
שמע יהוה וחנני יהוה היה עזר לי׃ | 10 |
Sikia, Yahwe, na unihurumie! Yahwe, uwe msaidizi wangu.
הפכת מספדי למחול לי פתחת שקי ותאזרני שמחה׃ | 11 |
Wewe umegeuza kuomboleza kwangu kuwa kucheza; wewe umeyaondoa mavazi yangu ya magunia na kunivisha furaha.
למען יזמרך כבוד ולא ידם יהוה אלהי לעולם אודך׃ | 12 |
Hivyo sasa utukufu wangu utakuimbia sifa wewe na hautanyamaza; Yahwe Mungu wangu, nitakushukuru wewe milele!