< תהילים 30 >

מזמור שיר חנכת הבית לדוד ארוממך יהוה כי דליתני ולא שמחת איבי לי׃ 1
Nitakutukuza wewe, Yahwe, kwa kuwa umeniinua na haujawaruhusu maadui zangu juu yangu.
יהוה אלהי שועתי אליך ותרפאני׃ 2
Yahwe Mungu wangu, nilikulilia wewe kwa ajili ya msaada, nawe ukaniponya.
יהוה העלית מן שאול נפשי חייתני מיורדי בור׃ (Sheol h7585) 3
Yahwe, wewe umeitoa roho yangu kuzimuni; nawe umeniweka hai mbali na kaburi. (Sheol h7585)
זמרו ליהוה חסידיו והודו לזכר קדשו׃ 4
Mwimbieni sifa Yahwe, ninyi waaminifu wake! Mshukuruni Bwana mkumbukapo utakatifu wake.
כי רגע באפו חיים ברצונו בערב ילין בכי ולבקר רנה׃ 5
Kwa kuwa hasira yake ni ya muda tu; bali neema yake yadumu milele. Kilio huja usiku, bali furaha huja asubuhi.
ואני אמרתי בשלוי בל אמוט לעולם׃ 6
Kwa ujasiri nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
יהוה ברצונך העמדתה להררי עז הסתרת פניך הייתי נבהל׃ 7
Yahwe, kwa neema yako uliniweka mimi kama mlima imara; lakini ulipouficha uso wako, nilisumbuka.
אליך יהוה אקרא ואל אדני אתחנן׃ 8
Nilikulilia wewe, Yahwe, na kuomba msaada kwa Bwana wangu!
מה בצע בדמי ברדתי אל שחת היודך עפר היגיד אמתך׃ 9
Kuna faida gani katika kifo changu, kama nitaenda kaburini? Je, mavumbi yatakusifu wewe? Yatatangaza uaminifu wako?
שמע יהוה וחנני יהוה היה עזר לי׃ 10
Sikia, Yahwe, na unihurumie! Yahwe, uwe msaidizi wangu.
הפכת מספדי למחול לי פתחת שקי ותאזרני שמחה׃ 11
Wewe umegeuza kuomboleza kwangu kuwa kucheza; wewe umeyaondoa mavazi yangu ya magunia na kunivisha furaha.
למען יזמרך כבוד ולא ידם יהוה אלהי לעולם אודך׃ 12
Hivyo sasa utukufu wangu utakuimbia sifa wewe na hautanyamaza; Yahwe Mungu wangu, nitakushukuru wewe milele!

< תהילים 30 >