< תהילים 27 >
לדוד יהוה אורי וישעי ממי אירא יהוה מעוז חיי ממי אפחד׃ | 1 |
Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
בקרב עלי מרעים לאכל את בשרי צרי ואיבי לי המה כשלו ונפלו׃ | 2 |
Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
אם תחנה עלי מחנה לא יירא לבי אם תקום עלי מלחמה בזאת אני בוטח׃ | 3 |
Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
אחת שאלתי מאת יהוה אותה אבקש שבתי בבית יהוה כל ימי חיי לחזות בנעם יהוה ולבקר בהיכלו׃ | 4 |
Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
כי יצפנני בסכה ביום רעה יסתרני בסתר אהלו בצור ירוממני׃ | 5 |
Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
ועתה ירום ראשי על איבי סביבותי ואזבחה באהלו זבחי תרועה אשירה ואזמרה ליהוה׃ | 6 |
Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
שמע יהוה קולי אקרא וחנני וענני׃ | 7 |
Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
לך אמר לבי בקשו פני את פניך יהוה אבקש׃ | 8 |
Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
אל תסתר פניך ממני אל תט באף עבדך עזרתי היית אל תטשני ואל תעזבני אלהי ישעי׃ | 9 |
Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
כי אבי ואמי עזבוני ויהוה יאספני׃ | 10 |
Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
הורני יהוה דרכך ונחני בארח מישור למען שוררי׃ | 11 |
Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
אל תתנני בנפש צרי כי קמו בי עדי שקר ויפח חמס׃ | 12 |
Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
לולא האמנתי לראות בטוב יהוה בארץ חיים׃ | 13 |
Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
קוה אל יהוה חזק ויאמץ לבך וקוה אל יהוה׃ | 14 |
Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!