< תהילים 27 >

לדוד יהוה אורי וישעי ממי אירא יהוה מעוז חיי ממי אפחד׃ 1
Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
בקרב עלי מרעים לאכל את בשרי צרי ואיבי לי המה כשלו ונפלו׃ 2
Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
אם תחנה עלי מחנה לא יירא לבי אם תקום עלי מלחמה בזאת אני בוטח׃ 3
Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
אחת שאלתי מאת יהוה אותה אבקש שבתי בבית יהוה כל ימי חיי לחזות בנעם יהוה ולבקר בהיכלו׃ 4
Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
כי יצפנני בסכה ביום רעה יסתרני בסתר אהלו בצור ירוממני׃ 5
Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
ועתה ירום ראשי על איבי סביבותי ואזבחה באהלו זבחי תרועה אשירה ואזמרה ליהוה׃ 6
Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
שמע יהוה קולי אקרא וחנני וענני׃ 7
Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
לך אמר לבי בקשו פני את פניך יהוה אבקש׃ 8
Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
אל תסתר פניך ממני אל תט באף עבדך עזרתי היית אל תטשני ואל תעזבני אלהי ישעי׃ 9
Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
כי אבי ואמי עזבוני ויהוה יאספני׃ 10
Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
הורני יהוה דרכך ונחני בארח מישור למען שוררי׃ 11
Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
אל תתנני בנפש צרי כי קמו בי עדי שקר ויפח חמס׃ 12
Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
לולא האמנתי לראות בטוב יהוה בארץ חיים׃ 13
Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
קוה אל יהוה חזק ויאמץ לבך וקוה אל יהוה׃ 14
Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!

< תהילים 27 >