< תהילים 25 >
לדוד אליך יהוה נפשי אשא׃ | 1 |
Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
אלהי בך בטחתי אל אבושה אל יעלצו איבי לי׃ | 2 |
Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
גם כל קויך לא יבשו יבשו הבוגדים ריקם׃ | 3 |
Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
דרכיך יהוה הודיעני ארחותיך למדני׃ | 4 |
Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
הדריכני באמתך ולמדני כי אתה אלהי ישעי אותך קויתי כל היום׃ | 5 |
Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
זכר רחמיך יהוה וחסדיך כי מעולם המה׃ | 6 |
Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
חטאות נעורי ופשעי אל תזכר כחסדך זכר לי אתה למען טובך יהוה׃ | 7 |
Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
טוב וישר יהוה על כן יורה חטאים בדרך׃ | 8 |
Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
ידרך ענוים במשפט וילמד ענוים דרכו׃ | 9 |
Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
כל ארחות יהוה חסד ואמת לנצרי בריתו ועדתיו׃ | 10 |
Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
למען שמך יהוה וסלחת לעוני כי רב הוא׃ | 11 |
Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
מי זה האיש ירא יהוה יורנו בדרך יבחר׃ | 12 |
Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
נפשו בטוב תלין וזרעו יירש ארץ׃ | 13 |
Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
סוד יהוה ליראיו ובריתו להודיעם׃ | 14 |
Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
עיני תמיד אל יהוה כי הוא יוציא מרשת רגלי׃ | 15 |
Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
פנה אלי וחנני כי יחיד ועני אני׃ | 16 |
Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
צרות לבבי הרחיבו ממצוקותי הוציאני׃ | 17 |
Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
ראה עניי ועמלי ושא לכל חטאותי׃ | 18 |
Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
ראה אויבי כי רבו ושנאת חמס שנאוני׃ | 19 |
Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
שמרה נפשי והצילני אל אבוש כי חסיתי בך׃ | 20 |
Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
תם וישר יצרוני כי קויתיך׃ | 21 |
Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
פדה אלהים את ישראל מכל צרותיו׃ | 22 |
Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!