< תהילים 25 >

לדוד אליך יהוה נפשי אשא׃ 1
Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
אלהי בך בטחתי אל אבושה אל יעלצו איבי לי׃ 2
Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
גם כל קויך לא יבשו יבשו הבוגדים ריקם׃ 3
Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
דרכיך יהוה הודיעני ארחותיך למדני׃ 4
Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
הדריכני באמתך ולמדני כי אתה אלהי ישעי אותך קויתי כל היום׃ 5
Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
זכר רחמיך יהוה וחסדיך כי מעולם המה׃ 6
Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
חטאות נעורי ופשעי אל תזכר כחסדך זכר לי אתה למען טובך יהוה׃ 7
Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
טוב וישר יהוה על כן יורה חטאים בדרך׃ 8
Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
ידרך ענוים במשפט וילמד ענוים דרכו׃ 9
Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
כל ארחות יהוה חסד ואמת לנצרי בריתו ועדתיו׃ 10
Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
למען שמך יהוה וסלחת לעוני כי רב הוא׃ 11
Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
מי זה האיש ירא יהוה יורנו בדרך יבחר׃ 12
Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
נפשו בטוב תלין וזרעו יירש ארץ׃ 13
Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
סוד יהוה ליראיו ובריתו להודיעם׃ 14
Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
עיני תמיד אל יהוה כי הוא יוציא מרשת רגלי׃ 15
Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
פנה אלי וחנני כי יחיד ועני אני׃ 16
Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
צרות לבבי הרחיבו ממצוקותי הוציאני׃ 17
Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
ראה עניי ועמלי ושא לכל חטאותי׃ 18
Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
ראה אויבי כי רבו ושנאת חמס שנאוני׃ 19
Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
שמרה נפשי והצילני אל אבוש כי חסיתי בך׃ 20
Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
תם וישר יצרוני כי קויתיך׃ 21
Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
פדה אלהים את ישראל מכל צרותיו׃ 22
Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!

< תהילים 25 >