< תהילים 21 >

למנצח מזמור לדוד יהוה בעזך ישמח מלך ובישועתך מה יגיל מאד׃ 1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, mfalme huzifurahia nguvu zako. Tazama jinsi ilivyo kuu furaha yake kwa ushindi unaompa!
תאות לבו נתתה לו וארשת שפתיו בל מנעת סלה׃ 2
Umempa haja ya moyo wake na hukumzuilia maombi ya midomo yake.
כי תקדמנו ברכות טוב תשית לראשו עטרת פז׃ 3
Ulimkaribisha kwa baraka tele na kumvika taji ya dhahabu safi kichwani pake.
חיים שאל ממך נתתה לו ארך ימים עולם ועד׃ 4
Alikuomba maisha, nawe ukampa, wingi wa siku milele na milele.
גדול כבודו בישועתך הוד והדר תשוה עליו׃ 5
Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa, umeweka juu yake fahari na utukufu.
כי תשיתהו ברכות לעד תחדהו בשמחה את פניך׃ 6
Hakika umempa baraka za milele, umemfanya awe na furaha kwa shangwe ya uwepo wako.
כי המלך בטח ביהוה ובחסד עליון בל ימוט׃ 7
Kwa kuwa mfalme anamtumaini Bwana; kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa.
תמצא ידך לכל איביך ימינך תמצא שנאיך׃ 8
Mkono wako utawashika adui zako wote, mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.
תשיתמו כתנור אש לעת פניך יהוה באפו יבלעם ותאכלם אש׃ 9
Wakati utakapojitokeza utawafanya kama tanuru ya moto. Katika ghadhabu yake Bwana atawameza, moto wake utawateketeza.
פרימו מארץ תאבד וזרעם מבני אדם׃ 10
Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani, uzao wao kutoka wanadamu.
כי נטו עליך רעה חשבו מזמה בל יוכלו׃ 11
Ingawa watapanga mabaya dhidi yako na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,
כי תשיתמו שכם במיתריך תכונן על פניהם׃ 12
kwa kuwa utawafanya wakimbie utakapowalenga usoni pao kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.
רומה יהוה בעזך נשירה ונזמרה גבורתך׃ 13
Ee Bwana, utukuzwe katika nguvu zako, tutaimba na kusifu nguvu zako.

< תהילים 21 >