< תהילים 2 >
למה רגשו גוים ולאמים יהגו ריק׃ | 1 |
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
יתיצבו מלכי ארץ ורוזנים נוסדו יחד על יהוה ועל משיחו׃ | 2 |
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
ננתקה את מוסרותימו ונשליכה ממנו עבתימו׃ | 3 |
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
יושב בשמים ישחק אדני ילעג למו׃ | 4 |
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
אז ידבר אלימו באפו ובחרונו יבהלמו׃ | 5 |
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
ואני נסכתי מלכי על ציון הר קדשי׃ | 6 |
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
אספרה אל חק יהוה אמר אלי בני אתה אני היום ילדתיך׃ | 7 |
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
שאל ממני ואתנה גוים נחלתך ואחזתך אפסי ארץ׃ | 8 |
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
תרעם בשבט ברזל ככלי יוצר תנפצם׃ | 9 |
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
ועתה מלכים השכילו הוסרו שפטי ארץ׃ | 10 |
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
עבדו את יהוה ביראה וגילו ברעדה׃ | 11 |
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
נשקו בר פן יאנף ותאבדו דרך כי יבער כמעט אפו אשרי כל חוסי בו׃ | 12 |
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.