< תהילים 132 >
שיר המעלות זכור יהוה לדוד את כל ענותו׃ | 1 |
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
אשר נשבע ליהוה נדר לאביר יעקב׃ | 2 |
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
אם אבא באהל ביתי אם אעלה על ערש יצועי׃ | 3 |
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
אם אתן שנת לעיני לעפעפי תנומה׃ | 4 |
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
עד אמצא מקום ליהוה משכנות לאביר יעקב׃ | 5 |
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
הנה שמענוה באפרתה מצאנוה בשדי יער׃ | 6 |
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
נבואה למשכנותיו נשתחוה להדם רגליו׃ | 7 |
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
קומה יהוה למנוחתך אתה וארון עזך׃ | 8 |
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
כהניך ילבשו צדק וחסידיך ירננו׃ | 9 |
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
בעבור דוד עבדך אל תשב פני משיחך׃ | 10 |
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
נשבע יהוה לדוד אמת לא ישוב ממנה מפרי בטנך אשית לכסא לך׃ | 11 |
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
אם ישמרו בניך בריתי ועדתי זו אלמדם גם בניהם עדי עד ישבו לכסא לך׃ | 12 |
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
כי בחר יהוה בציון אוה למושב לו׃ | 13 |
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
זאת מנוחתי עדי עד פה אשב כי אותיה׃ | 14 |
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
צידה ברך אברך אביוניה אשביע לחם׃ | 15 |
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
וכהניה אלביש ישע וחסידיה רנן ירננו׃ | 16 |
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
שם אצמיח קרן לדוד ערכתי נר למשיחי׃ | 17 |
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
אויביו אלביש בשת ועליו יציץ נזרו׃ | 18 |
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”