< תהילים 129 >
שיר המעלות רבת צררוני מנעורי יאמר נא ישראל׃ | 1 |
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
רבת צררוני מנעורי גם לא יכלו לי׃ | 2 |
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
על גבי חרשו חרשים האריכו למענותם׃ | 3 |
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
יהוה צדיק קצץ עבות רשעים׃ | 4 |
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
יבשו ויסגו אחור כל שנאי ציון׃ | 5 |
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
יהיו כחציר גגות שקדמת שלף יבש׃ | 6 |
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
שלא מלא כפו קוצר וחצנו מעמר׃ | 7 |
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
ולא אמרו העברים ברכת יהוה אליכם ברכנו אתכם בשם יהוה׃ | 8 |
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”