< תהילים 121 >

שיר למעלות אשא עיני אל ההרים מאין יבא עזרי׃ 1
Wimbo wa kwenda juu. Nayainua macho yangu nitazame vilima, msaada wangu utatoka wapi?
עזרי מעם יהוה עשה שמים וארץ׃ 2
Msaada wangu hutoka kwa Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
אל יתן למוט רגלך אל ינום שמרך׃ 3
Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,
הנה לא ינום ולא יישן שומר ישראל׃ 4
hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.
יהוה שמרך יהוה צלך על יד ימינך׃ 5
Bwana anakulinda, Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
יומם השמש לא יככה וירח בלילה׃ 6
jua halitakudhuru mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
יהוה ישמרך מכל רע ישמר את נפשך׃ 7
Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako,
יהוה ישמר צאתך ובואך מעתה ועד עולם׃ 8
Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.

< תהילים 121 >