< תהילים 119 >
אשרי תמימי דרך ההלכים בתורת יהוה׃ | 1 |
Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
אשרי נצרי עדתיו בכל לב ידרשוהו׃ | 2 |
Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
אף לא פעלו עולה בדרכיו הלכו׃ | 3 |
Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.
אתה צויתה פקדיך לשמר מאד׃ | 4 |
Umetoa maagizo yako ili tuyatii kwa ukamilifu.
אחלי יכנו דרכי לשמר חקיך׃ | 5 |
Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako!
אז לא אבוש בהביטי אל כל מצותיך׃ | 6 |
Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote.
אודך בישר לבב בלמדי משפטי צדקך׃ | 7 |
Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki.
את חקיך אשמר אל תעזבני עד מאד׃ | 8 |
Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.
במה יזכה נער את ארחו לשמר כדברך׃ | 9 |
Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani? Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.
בכל לבי דרשתיך אל תשגני ממצותיך׃ | 10 |
Ninakutafuta kwa moyo wangu wote, usiniache niende mbali na amri zako.
בלבי צפנתי אמרתך למען לא אחטא לך׃ | 11 |
Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi.
ברוך אתה יהוה למדני חקיך׃ | 12 |
Sifa ni zako, Ee Bwana, nifundishe maagizo yako.
בשפתי ספרתי כל משפטי פיך׃ | 13 |
Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote zinazotoka katika kinywa chako.
בדרך עדותיך ששתי כעל כל הון׃ | 14 |
Ninafurahia kufuata sheria zako kama mtu afurahiaye mali nyingi.
בפקדיך אשיחה ואביטה ארחתיך׃ | 15 |
Ninatafakari maagizo yako na kuziangalia njia zako.
בחקתיך אשתעשע לא אשכח דברך׃ | 16 |
Ninafurahia maagizo yako, wala sitalipuuza neno lako.
גמל על עבדך אחיה ואשמרה דברך׃ | 17 |
Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi; nitalitii neno lako.
גל עיני ואביטה נפלאות מתורתך׃ | 18 |
Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
גר אנכי בארץ אל תסתר ממני מצותיך׃ | 19 |
Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako.
גרסה נפשי לתאבה אל משפטיך בכל עת׃ | 20 |
Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa juu ya sheria zako wakati wote.
גערת זדים ארורים השגים ממצותיך׃ | 21 |
Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.
גל מעלי חרפה ובוז כי עדתיך נצרתי׃ | 22 |
Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako.
גם ישבו שרים בי נדברו עבדך ישיח בחקיך׃ | 23 |
Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
גם עדתיך שעשעי אנשי עצתי׃ | 24 |
Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu.
דבקה לעפר נפשי חיני כדברך׃ | 25 |
Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
דרכי ספרתי ותענני למדני חקיך׃ | 26 |
Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.
דרך פקודיך הבינני ואשיחה בנפלאותיך׃ | 27 |
Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
דלפה נפשי מתוגה קימני כדברך׃ | 28 |
Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
דרך שקר הסר ממני ותורתך חנני׃ | 29 |
Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
דרך אמונה בחרתי משפטיך שויתי׃ | 30 |
Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
דבקתי בעדותיך יהוה אל תבישני׃ | 31 |
Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana, usiniache niaibishwe.
דרך מצותיך ארוץ כי תרחיב לבי׃ | 32 |
Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.
הורני יהוה דרך חקיך ואצרנה עקב׃ | 33 |
Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho.
הבינני ואצרה תורתך ואשמרנה בכל לב׃ | 34 |
Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote.
הדריכני בנתיב מצותיך כי בו חפצתי׃ | 35 |
Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha.
הט לבי אל עדותיך ואל אל בצע׃ | 36 |
Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
העבר עיני מראות שוא בדרכך חיני׃ | 37 |
Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
הקם לעבדך אמרתך אשר ליראתך׃ | 38 |
Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa.
העבר חרפתי אשר יגרתי כי משפטיך טובים׃ | 39 |
Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema.
הנה תאבתי לפקדיך בצדקתך חיני׃ | 40 |
Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.
ויבאני חסדך יהוה תשועתך כאמרתך׃ | 41 |
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
ואענה חרפי דבר כי בטחתי בדברך׃ | 42 |
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
ואל תצל מפי דבר אמת עד מאד כי למשפטך יחלתי׃ | 43 |
Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
ואשמרה תורתך תמיד לעולם ועד׃ | 44 |
Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
ואתהלכה ברחבה כי פקדיך דרשתי׃ | 45 |
Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
ואדברה בעדתיך נגד מלכים ולא אבוש׃ | 46 |
Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,
ואשתעשע במצותיך אשר אהבתי׃ | 47 |
kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.
ואשא כפי אל מצותיך אשר אהבתי ואשיחה בחקיך׃ | 48 |
Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.
זכר דבר לעבדך על אשר יחלתני׃ | 49 |
Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.
זאת נחמתי בעניי כי אמרתך חיתני׃ | 50 |
Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
זדים הליצני עד מאד מתורתך לא נטיתי׃ | 51 |
Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.
זכרתי משפטיך מעולם יהוה ואתנחם׃ | 52 |
Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.
זלעפה אחזתני מרשעים עזבי תורתך׃ | 53 |
Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.
זמרות היו לי חקיך בבית מגורי׃ | 54 |
Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.
זכרתי בלילה שמך יהוה ואשמרה תורתך׃ | 55 |
Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako.
זאת היתה לי כי פקדיך נצרתי׃ | 56 |
Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.
חלקי יהוה אמרתי לשמר דבריך׃ | 57 |
Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.
חליתי פניך בכל לב חנני כאמרתך׃ | 58 |
Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.
חשבתי דרכי ואשיבה רגלי אל עדתיך׃ | 59 |
Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
חשתי ולא התמהמהתי לשמר מצותיך׃ | 60 |
Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
חבלי רשעים עודני תורתך לא שכחתי׃ | 61 |
Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.
חצות לילה אקום להודות לך על משפטי צדקך׃ | 62 |
Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.
חבר אני לכל אשר יראוך ולשמרי פקודיך׃ | 63 |
Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.
חסדך יהוה מלאה הארץ חקיך למדני׃ | 64 |
Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.
טוב עשית עם עבדך יהוה כדברך׃ | 65 |
Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
טוב טעם ודעת למדני כי במצותיך האמנתי׃ | 66 |
Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.
טרם אענה אני שגג ועתה אמרתך שמרתי׃ | 67 |
Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.
טוב אתה ומטיב למדני חקיך׃ | 68 |
Wewe ni mwema, unalotenda ni jema, nifundishe maagizo yako.
טפלו עלי שקר זדים אני בכל לב אצר פקודיך׃ | 69 |
Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.
טפש כחלב לבם אני תורתך שעשעתי׃ | 70 |
Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.
טוב לי כי עניתי למען אלמד חקיך׃ | 71 |
Ilikuwa vyema mimi kupata shida ili nipate kujifunza maagizo yako.
טוב לי תורת פיך מאלפי זהב וכסף׃ | 72 |
Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.
ידיך עשוני ויכוננוני הבינני ואלמדה מצותיך׃ | 73 |
Mikono yako ilinifanya na kuniumba, nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
יראיך יראוני וישמחו כי לדברך יחלתי׃ | 74 |
Wakuchao wafurahie wanaponiona, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
ידעתי יהוה כי צדק משפטיך ואמונה עניתני׃ | 75 |
Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.
יהי נא חסדך לנחמני כאמרתך לעבדך׃ | 76 |
Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu, sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
יבאוני רחמיך ואחיה כי תורתך שעשעי׃ | 77 |
Huruma yako na inijie ili nipate kuishi, kwa kuwa naifurahia sheria yako.
יבשו זדים כי שקר עותוני אני אשיח בפקודיך׃ | 78 |
Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
ישובו לי יראיך וידעו עדתיך׃ | 79 |
Wale wakuchao na wanigeukie mimi, hao ambao wanazielewa sheria zako.
יהי לבי תמים בחקיך למען לא אבוש׃ | 80 |
Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako, ili nisiaibishwe.
כלתה לתשועתך נפשי לדברך יחלתי׃ | 81 |
Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.
כלו עיני לאמרתך לאמר מתי תנחמני׃ | 82 |
Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifajiri lini?”
כי הייתי כנאד בקיטור חקיך לא שכחתי׃ | 83 |
Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi, bado sijasahau maagizo yako.
כמה ימי עבדך מתי תעשה ברדפי משפט׃ | 84 |
Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini? Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?
כרו לי זדים שיחות אשר לא כתורתך׃ | 85 |
Wenye majivuno wananichimbia mashimo, kinyume na sheria yako.
כל מצותיך אמונה שקר רדפוני עזרני׃ | 86 |
Amri zako zote ni za kuaminika; unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.
כמעט כלוני בארץ ואני לא עזבתי פקודיך׃ | 87 |
Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia, lakini sijaacha mausia yako.
כחסדך חיני ואשמרה עדות פיך׃ | 88 |
Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako, nami nitatii sheria za kinywa chako.
לעולם יהוה דברך נצב בשמים׃ | 89 |
Ee Bwana, neno lako ni la milele, linasimama imara mbinguni.
לדר ודר אמונתך כוננת ארץ ותעמד׃ | 90 |
Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote, umeiumba dunia, nayo inadumu.
למשפטיך עמדו היום כי הכל עבדיך׃ | 91 |
Sheria zako zinadumu hadi leo, kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
לולי תורתך שעשעי אז אבדתי בעניי׃ | 92 |
Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.
לעולם לא אשכח פקודיך כי בם חייתני׃ | 93 |
Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
לך אני הושיעני כי פקודיך דרשתי׃ | 94 |
Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
לי קוו רשעים לאבדני עדתיך אתבונן׃ | 95 |
Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
לכל תכלה ראיתי קץ רחבה מצותך מאד׃ | 96 |
Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
מה אהבתי תורתך כל היום היא שיחתי׃ | 97 |
Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
מאיבי תחכמני מצותך כי לעולם היא לי׃ | 98 |
Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
מכל מלמדי השכלתי כי עדותיך שיחה לי׃ | 99 |
Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
מזקנים אתבונן כי פקודיך נצרתי׃ | 100 |
Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
מכל ארח רע כלאתי רגלי למען אשמר דברך׃ | 101 |
Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
ממשפטיך לא סרתי כי אתה הורתני׃ | 102 |
Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
מה נמלצו לחכי אמרתך מדבש לפי׃ | 103 |
Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
מפקודיך אתבונן על כן שנאתי כל ארח שקר׃ | 104 |
Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
נר לרגלי דברך ואור לנתיבתי׃ | 105 |
Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
נשבעתי ואקימה לשמר משפטי צדקך׃ | 106 |
Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
נעניתי עד מאד יהוה חיני כדברך׃ | 107 |
Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
נדבות פי רצה נא יהוה ומשפטיך למדני׃ | 108 |
Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
נפשי בכפי תמיד ותורתך לא שכחתי׃ | 109 |
Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
נתנו רשעים פח לי ומפקודיך לא תעיתי׃ | 110 |
Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
נחלתי עדותיך לעולם כי ששון לבי המה׃ | 111 |
Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
נטיתי לבי לעשות חקיך לעולם עקב׃ | 112 |
Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
סעפים שנאתי ותורתך אהבתי׃ | 113 |
Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
סתרי ומגני אתה לדברך יחלתי׃ | 114 |
Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
סורו ממני מרעים ואצרה מצות אלהי׃ | 115 |
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
סמכני כאמרתך ואחיה ואל תבישני משברי׃ | 116 |
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
סעדני ואושעה ואשעה בחקיך תמיד׃ | 117 |
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.
סלית כל שוגים מחקיך כי שקר תרמיתם׃ | 118 |
Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako, kwa maana udanganyifu wao ni bure.
סגים השבת כל רשעי ארץ לכן אהבתי עדתיך׃ | 119 |
Waovu wa nchi unawatupa kama takataka, kwa hivyo nazipenda sheria zako.
סמר מפחדך בשרי וממשפטיך יראתי׃ | 120 |
Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe, ninaziogopa sheria zako.
עשיתי משפט וצדק בל תניחני לעשקי׃ | 121 |
Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
ערב עבדך לטוב אל יעשקני זדים׃ | 122 |
Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
עיני כלו לישועתך ולאמרת צדקך׃ | 123 |
Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
עשה עם עבדך כחסדך וחקיך למדני׃ | 124 |
Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
עבדך אני הבינני ואדעה עדתיך׃ | 125 |
Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
עת לעשות ליהוה הפרו תורתך׃ | 126 |
Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.
על כן אהבתי מצותיך מזהב ומפז׃ | 127 |
Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu, naam, zaidi ya dhahabu safi,
על כן כל פקודי כל ישרתי כל ארח שקר שנאתי׃ | 128 |
na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili, nachukia kila njia potovu.
פלאות עדותיך על כן נצרתם נפשי׃ | 129 |
Sheria zako ni za ajabu, hivyo ninazitii.
פתח דבריך יאיר מבין פתיים׃ | 130 |
Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru, kunampa mjinga ufahamu.
פי פערתי ואשאפה כי למצותיך יאבתי׃ | 131 |
Nimefungua kinywa changu na kuhema, nikitamani amri zako.
פנה אלי וחנני כמשפט לאהבי שמך׃ | 132 |
Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote wale wanaolipenda jina lako.
פעמי הכן באמרתך ואל תשלט בי כל און׃ | 133 |
Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako, usiache dhambi yoyote initawale.
פדני מעשק אדם ואשמרה פקודיך׃ | 134 |
Niokoe na uonevu wa wanadamu, ili niweze kutii mausia yako.
פניך האר בעבדך ולמדני את חקיך׃ | 135 |
Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
פלגי מים ירדו עיני על לא שמרו תורתך׃ | 136 |
Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
צדיק אתה יהוה וישר משפטיך׃ | 137 |
Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
צוית צדק עדתיך ואמונה מאד׃ | 138 |
Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
צמתתני קנאתי כי שכחו דבריך צרי׃ | 139 |
Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
צרופה אמרתך מאד ועבדך אהבה׃ | 140 |
Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
צעיר אנכי ונבזה פקדיך לא שכחתי׃ | 141 |
Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
צדקתך צדק לעולם ותורתך אמת׃ | 142 |
Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
צר ומצוק מצאוני מצותיך שעשעי׃ | 143 |
Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
צדק עדותיך לעולם הבינני ואחיה׃ | 144 |
Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
קראתי בכל לב ענני יהוה חקיך אצרה׃ | 145 |
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
קראתיך הושיעני ואשמרה עדתיך׃ | 146 |
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
קדמתי בנשף ואשועה לדבריך יחלתי׃ | 147 |
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
קדמו עיני אשמרות לשיח באמרתך׃ | 148 |
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
קולי שמעה כחסדך יהוה כמשפטך חיני׃ | 149 |
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
קרבו רדפי זמה מתורתך רחקו׃ | 150 |
Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
קרוב אתה יהוה וכל מצותיך אמת׃ | 151 |
Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
קדם ידעתי מעדתיך כי לעולם יסדתם׃ | 152 |
Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
ראה עניי וחלצני כי תורתך לא שכחתי׃ | 153 |
Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako.
ריבה ריבי וגאלני לאמרתך חיני׃ | 154 |
Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
רחוק מרשעים ישועה כי חקיך לא דרשו׃ | 155 |
Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
רחמיך רבים יהוה כמשפטיך חיני׃ | 156 |
Ee Bwana, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
רבים רדפי וצרי מעדותיך לא נטיתי׃ | 157 |
Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako.
ראיתי בגדים ואתקוטטה אשר אמרתך לא שמרו׃ | 158 |
Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako.
ראה כי פקודיך אהבתי יהוה כחסדך חיני׃ | 159 |
Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.
ראש דברך אמת ולעולם כל משפט צדקך׃ | 160 |
Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.
שרים רדפוני חנם ומדבריך פחד לבי׃ | 161 |
Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
שש אנכי על אמרתך כמוצא שלל רב׃ | 162 |
Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
שקר שנאתי ואתעבה תורתך אהבתי׃ | 163 |
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
שבע ביום הללתיך על משפטי צדקך׃ | 164 |
Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
שלום רב לאהבי תורתך ואין למו מכשול׃ | 165 |
Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
שברתי לישועתך יהוה ומצותיך עשיתי׃ | 166 |
Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
שמרה נפשי עדתיך ואהבם מאד׃ | 167 |
Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
שמרתי פקודיך ועדתיך כי כל דרכי נגדך׃ | 168 |
Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
תקרב רנתי לפניך יהוה כדברך הבינני׃ | 169 |
Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako, nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
תבוא תחנתי לפניך כאמרתך הצילני׃ | 170 |
Maombi yangu na yafike mbele zako, niokoe sawasawa na ahadi yako.
תבענה שפתי תהלה כי תלמדני חקיך׃ | 171 |
Midomo yangu na ibubujike sifa, kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
תען לשוני אמרתך כי כל מצותיך צדק׃ | 172 |
Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
תהי ידך לעזרני כי פקודיך בחרתי׃ | 173 |
Mkono wako uwe tayari kunisaidia, kwa kuwa nimechagua mausia yako.
תאבתי לישועתך יהוה ותורתך שעשעי׃ | 174 |
Ee Bwana, ninatamani wokovu wako, na sheria yako ni furaha yangu.
תחי נפשי ותהללך ומשפטך יעזרני׃ | 175 |
Nijalie kuishi ili nipate kukusifu, na sheria zako zinitegemeze.
תעיתי כשה אבד בקש עבדך כי מצותיך לא שכחתי׃ | 176 |
Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.